Na WINNIE ATIENO
MBUNGE wa Likoni Bi Mishi Mboko amejiondoa kwenye kinyang’anyiro cha ugavana wa Mombasa.
Bi Mboko ambaye alikuwa mgombea mwanamke wa kipekee katika kinyang’anyiro hicho alisema atatetea kiti chake cha Ubunge akiwataka wakazi wa Likoni kumuunga mkono.
“Ninataka kuwakumbusha kwamba nitagombania kiti cha Ubunge wa Likoni nimefanya kazi nzuri na mkiamua kunirejesha bungeni nitashukuru. Ninachohitaji ni muniunge mkono, siwezi kuendelea safari hii peke yangu,” alisema.