• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 9:12 AM
Napoli waajiri kocha Rudi Garcia kujaza pengo la Luciano Spalletti

Napoli waajiri kocha Rudi Garcia kujaza pengo la Luciano Spalletti

Na MASHIRIKA

MABINGWA wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A), Napoli, wameajiri kocha mpya, Rudi Garcia.

Mkufunzi huyo raia wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 59 anajaza nafasi ya Luciano Spalletti aliyeagana rasmi na Napoli baada ya kuwaongoza kujinyanyulia taji la kwanza la Serie A mnamo Mei 2023 baada ya subira ya miaka 33.

Sawa na Spalletti, Garcia naye aliwahi kudhibiti mikoba ya AS Roma katika Serie A na akasaidia Lille kushinda taji la Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) na French Cup mnamo 2010-11.

Baada ya kuhudumu kambini mwa Olympique Marseille na Olympique Lyon, kikosi cha hivi karibuni zaidi kwa Garcia kunoa ni Al Nassr cha Ligi Kuu ya Saudi Arabia. Alikatiza uhusiano wake na klabu hiyo mnamo Aprili 2023.

“Nina fahari ya kutangaza kuwa nimekuwa katika mawasiliano ya mara kwa mara na Rudi Garcia katika kipindi cha siku 10 zilizopita. Tulikutana na amekubali kuwa kocha mpya wa Napoli,” akasema mmiliki wa kikosi hicho, Aurelio De Laurentiis.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

  • Tags

You can share this post!

Uhispania waangusha Italia na kujikatia tiketi ya kuvaana...

Tiba za nyumbani kwa kichefuchefu

T L