• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 11:14 AM
Paka ajumuika na waumini kwa swala ya Tarawehi

Paka ajumuika na waumini kwa swala ya Tarawehi

Na MASHIRIKA

ALGIERS, ALGERIA

KIOJA kilitokea nchini Algeria juzi paka alipopanda mabegani mwa Imam Sheikh Walid Mehsas wakati alipokuwa akiongoza maombi ya swala ndefu ya Tarawehi.

Maombi hayo hufanywa kila jioni katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Video iliyowekwa katika ukurasa wa Facebook wa kiongozi huyo wa kidini wa Kiislamu inamwonyesha akitulia na kumruhusu paka huyo kusimama mabegani mwake, bila kushtuka.

Sheikh Walid Mehsas aliendelea na maombi huku paka akionekana pia kuungana naye katika swala hiyo ya jioni.

Tafsiri: CHARLES WASONGA

  • Tags

You can share this post!

Handisheki yanukia, adokeza mwanauchumi David Ndii

Mashindano ya riadha kanda ya Kati yatia fora licha ya mvua

T L