Na MASHIRIKA
ALGIERS, ALGERIA
KIOJA kilitokea nchini Algeria juzi paka alipopanda mabegani mwa Imam Sheikh Walid Mehsas wakati alipokuwa akiongoza maombi ya swala ndefu ya Tarawehi.
Maombi hayo hufanywa kila jioni katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Video iliyowekwa katika ukurasa wa Facebook wa kiongozi huyo wa kidini wa Kiislamu inamwonyesha akitulia na kumruhusu paka huyo kusimama mabegani mwake, bila kushtuka.
Sheikh Walid Mehsas aliendelea na maombi huku paka akionekana pia kuungana naye katika swala hiyo ya jioni.
Tafsiri: CHARLES WASONGA