• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
PAMBO: Jinsi ya kumkolesha asali mchumba wako chumbani

PAMBO: Jinsi ya kumkolesha asali mchumba wako chumbani

Na BENSON MATHEKA

‘‘Unapombusu mwanadada, kuwa muungwana, fanya hivyo kwa heshima, usisukume ulimi wako ndani ya mdomo wake kana kwamba umepagawa, mleweshe kwa busu taratibu na kwa unyenyekevu.
-Joyce Kilavi
(Shirika la Make it Real)

 

IKIWA wewe ni mwanamume na unataka kuchukiwa na mchumba wako, basi mharakishe kushiriki tendo la ndoa, mpapase kwa pupa na kumpiga mabusu bila mpango.

Kulingana na utafiti wa gazeti la The Sun la Uingereza, wanawake huwachukia wanaume wanaojibwaga kwa shughuli bila mpango, wanaowaparamia wanawake kama simba wanaotafuna windo wakati wa njaa na wasioweza kuwakata kiu ya uroda.

“Ni makosa wanaume kuamini kwamba busu moja linatosha kumsukuma mwanamke kitandani kumega tunda. Hapana, ikiwa unaamini hivi, utatemwa na wanawake wote duniani na hakuna atakayekufungulia mzinga,” unasema utafiti uliochapishwa katika makala maarufu ya Fabulous kwenye gazeti hilo.

 

Epuka busu la fujo

Wanawake wengi walioshirikishwa kwenye utafiti huo walisema kwamba wanapenda wanaume wanaowabusu kwa unyenyekevu na sio wanaomumunya midomo na ulimi kwa fujo.

“Mwanamume anayefanya hivyo ni ibilisi katika masuala ya mapenzi, ni wale wanaojali ashiki zao pekee na sio hisia za wachumba wao,” anaeleza Joyce Kilavi wa Shirika la Make It Real jijini Nairobi.

Kulingana na vipusa waliohojiwa na The Sun, japo wanawake huwa wanasisimuliwa na mabusu motomoto haimaanishi ni ishara ya kuwa tayari kurushana roho.

Bi Kilavi anakubaliana na hili akisema wanaume huwa wanakosea kwa kuchukulia kuwa wanawake wakikubali uwabusu huwa wanalenga tendo la ndoa.

“Na unapombusu mwanadada, kuwa muungwana, fanya hivyo kwa heshima, usisukume ulimi wako ndani ya mdomo wake kana kwamba umepagawa. Vipusa huleweshwa na busu taratibu na kwa unyenyekevu,” asema.

 

Kuamsha hisia

Sawa na busu, wanawake wengi huchukia wanaume wasiojua kuamsha hisia zao kabla ya kulishana uroda. Walisema kwamba baadhi ya wanaume ni wabinafsi sana.

“Wanawake wengi walikasirishwa na tabia ya wanaume kutojali miili ya wachumba wao. Walisema wanaume wengi wana tabia ya kupenda kucheza ngoma yenyewe bila kufahamu tabia hiyo huwazima wanaume kabisa wakakosa hamu ya uroda,” unaeleza utafiti huo.

“Kumshughulikia mwanamke wakati wa uroda na kumfikisha kilele ni sanaa isiyohitaji pupa, fujo au ubinafsi. Inahitaji mtu anayeelewa mwili wa mchumba wake ipasavyo. Anayeelewa mwili wa mwanadada atafahamu akiwa tayari kwa ngoma,” asema Bi Kilavi.

 

Kupapasa na kutomasa

Wataalamu wanasema kwamba wanaume wanafaa kugutuka na kutumia muujiza wa kupapasa na kuwatomasa vipusa kwa ustadi na unyenyekevu. “Wanaoelewa kufanya hivi bila shaka wanajua mapenzi ya kuridhisha. Vipusa huwafuata,” unaeleza utafiti wa The Sun.

Kulingana na Bi Kilavi, mwanaume anayeelewa miujiza ya kupapasa vipusa hawezi kukaukiwa na uroda.

“Vipusa watatamani kuwa mikononi mwake kila wakati,” asema.

Kulingana na wataalamu makosa makubwa ya wanaume ni kuiga wanayotazama katika video za ngono na kufikiri kwamba wakifanya mapenzi kwa fujo, watawaridhisha wachumba wao.

 

Picha za uroda

“Hapana, wanayotazama katika picha za ngono sio mapenzi halisi kamwe, ni maigizo ya watu wanaopotosha wanaotazama vituko vyao,” asema Bw John Muriuki, mtaalamu wa masuala ya mapenzi wa shirika la Big Hearts jijini Nairobi.

Utafiti wa The Sun unaeleza kwamba wanaume huwachukiza vipusa wapenzi wao kwa kuwataka kubadilisha mbinu za uroda baada ya sekunde kadhaa wakiiga wanayotazama kwenye ponografia. “ Makeke katika uroda ni sawa, lakini ukiongeza chumvi kupita kiasi, unavuruga unaharibu ngoma,” unaeleza utafiti huo.

Wanawake wengi hutekwa kimapenzi na wanaume wanaofuatilia vituko vyao wakati wa shughuli na kuwachukia wale ambao haja yao ni kujiburudisha pekee.

“Kuna wanaume ambao hufunga macho na masikio yao wakati wa shughuli. Lengo lao huwa ni kufyatuka tu na hawajali hisia za wachumba wao. Wanawake huwa wanawachukia wanawake kama hao,” aeleza Bi Kilavi.

You can share this post!

FUNGUKA: ‘Paka wazee ndio shibe yangu’

Ramaphosa atimua mawaziri waliokuwa wandani wa Zuma

adminleo