• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Pombe haramu lita zaidi ya 300 yaharibiwa katika mitaa mitatu ya mabanda

Pombe haramu lita zaidi ya 300 yaharibiwa katika mitaa mitatu ya mabanda

Na SAMMY KIMATU

WASHUKIWA watatu walikamatwa huku lita zaidi ya 300 za pombe haramu zikiharibiwa katika mitaa mitatu ya mabanda, Kaunti ya Nairobi, Jumanne.

Aidha, msako huo ulifanyika katika mtaa wa mabanda wa Mukuru-Fuata Nyayo, Mariguini na Kisii kwenye maeneo ya South B, kaunti ndogo ya Starehe.

Msako huo uliongozwa na chifu wa eneo hilo, Bw Charles Mwatha, Naibuye Bw, Bw Paul Mulinge, maafisa wa polisi na viongozi wa Nyumba Kumi mtaani.

Chifu Mwatha aliambia Taifa Leo kwamba msako huo ulifanikiwa baada ya wakazi kushirikiana na kamati ya usalama mtaani.

“Msako wetu ulifaulu kwa sababu wananchi walishirikiana na kamati ya Nyumba Kumi mtaani kutupasha habari zozote zinazohusiana na usalama wa mitaa yetu,” Bw Mwatha akasema asema.

Wakati wa msako huo, pombe aina ya toivo, busaa na chang’aa zilinaswa na kuharibiwa huku milango ya nyumba ikibomolrewa na kubebwa.

Isitoshe, maafisa wa utawala waliharibu vifaa vilivyotumiwa kutengeneza pombe.

Fauka ya hayo, maafisa wa utawala walisema wauzaji wa pombe haramu walifanikiwa kutoroka baada ya kupashwa habari kuna msako.

Kufuatia mawasiliano kwa njia ya simu, polisi na machifu hawangeweza kupata stoo za pombe husika kwani pombe iliyonaswa ilikuwa ile iliyokuwa tayari kuuziwa wateja.

“Wauzaji wengi walifanikiwa kutoroka mtego wa machifu na polisi baada ya kupigiana simu. Hata hivyo, wajue chuma chao kimotoni kwani misako zaidi na itakayokuwa mikali imepangwa,’’ chifu Mwatha asema.

You can share this post!

Wanasoka wa Brazil wafuzu kwa robo-fainali za Olimpiki huku...

EACC yalaumiwa kwa kuhujumu juhudi za kukombolewa kwa fedha...