• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 11:14 AM
Raila Odinga Junior aitaka serikali ihalalishe bangi

Raila Odinga Junior aitaka serikali ihalalishe bangi

NA MWANDISHI WETU

MWANAWE aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga, Raila Junior ameitaka serikali kuwazia kuhalalisha matumizi ya bangi, ili kusaidia wafanyabiashara wa dawa hiyo ya kulevya ama watu wa dini wanaoitumia katika shughuli zao.

Raila Junior anasema kuna haja ya serikali kuangazia suala hilo kwa umuhimu na kwa haraka.

Mnamo 2015, Mbunge wa Kibra Ken Okoth aliwataka wakulima wa miwa kutoka magharibi mwa Kenya wakuze bangi badala ya zao hilo ambalo haliwaletei faida.

Mnamo 2016, Bw mtafiti Sammy Gwada Ogot aliwasilisha ombi katika seneti akitaka bangi ihalalishwe kwa misingi hiyo ya kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa.

You can share this post!

KRA yafunga akaunti za benki za FKF kwa kulemewa kulipa...

Wabunge wakaidi pendekezo la Uhuru

adminleo