• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Ugali ghali wabisha

Ugali ghali wabisha

Na BERNARDINE MUTANU

HUENDA gharama ya unga wa ugali ikaongezeka ikiwa mswada uliowasilishwa Bungeni utapitishwa na kuidhinishwa na rais.

Mswada huo ulifikishwa Bungeni miezi kadhaa iliyopita. Mswada huo wa Marekebisho ya Ushuru 2018 unalenga kubadilisha hadhi ya mahindi, ngano na mhogo, ambazo hazitozwi ushuru.

Kulingana na watengenezaji wa unga, kiwango cha ushuru kikibadilishwa kitapandisha bei ya unga, gharama itakayolimbikiziwa wateja wa unga.

“Hii ni kumaanisha kuwa watengenezaji wa unga hawawezi kujilipa ushuru unaotozwa bidhaa (VAT) kwa malighafi wanayotumia kutengeneza unga, kumaanisha kuwa gharama hiyo itapitishwa kwa wateja,” kilisema chama cha watengenezaji unga.

Bili hiyo inalenga mapato yanayotokana na unga wa mahindi, mkate na unga wa mhogo.

You can share this post!

Yaibuka Igathe anafaa zaidi kwa sekta ya benki

Kesi ya jaji aliyetupa kesi iliyomkabili Pattni kusikizwa...

adminleo