• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 12:26 PM
WIKI YA LUGHA ZA KIAFRIKA: Ukoloni ulivyochangia tabia ya kuzionea aibu lugha zetu za asili Kiswahili kikiwemo

WIKI YA LUGHA ZA KIAFRIKA: Ukoloni ulivyochangia tabia ya kuzionea aibu lugha zetu za asili Kiswahili kikiwemo

NA BITUGI MATUNDURA

MBONA tunaonea Kiswahili aibu ilhali ni lugha yetu asili?

Jibu kwa swali hili linapatikana katika kuitalii hali ya jinsi ambavyo wakoloni waliozuru bara la Afrika na kututawala walizichukulia lugha zetu za asili.

Wakoloni waliotawala Afrika ni pamoja na Wafaransa, Wajerumani na Waingereza. Mataifa mengi yaliyotawaliwa na Wafaransa na Waingereza bado yana mihuri ya lugha za watawala wao.

Mataifa mengi ya Afrika Magharibi hutumia Kifaransa kuwa ndiyo lugha yao rasmi (Benin, Ivory Coast, Guinea na Togo).

Nigeria, Ghana, Sierra Leone na Gambia hutumia Kiingereza kuwa lugha yao rasmi. Hali hii pia huonekana Afrika Mashariki na Kati na kusini mwa Afrika.

Wafaransa walisisitiza ukuzaji wa Kifaransa katika shule za maeneo waliyotawala.

Hii leo Chambacho mtaalamu Pierre Alexandre, wasomi wengi katika maeneo hayo wanajua Kifaransa kupindukia na wamezama katika utamaduni wa Wafaransa kuliko wanavyojua lugha na utamaduni wao.

Hata hivyo, hali ilikuwa tofauti katika himaya za Waingereza. Waingereza angalau walijihusisha na ukuzaji wa lugha za Kiafrika.

Wasomi wengi Waingereza walijifunza lugha na tamaduni za Waafrika na kuchapisha vitabu vingi kwa lugha hizo – zikiwemo kamusi na vitabu vya sarufi.

Huku wageni wakizama katika utafiti kuhusu lugha za wenyeji wao, Waafrika walizidharau lugha zao na kuziona kuwa ‘shenzi’ na za hadhi ya chini. Hatua ya kuadhimisha Wiki ya lugha za Kiafrika inafaa kuchangia mwamko mpya.

You can share this post!

NGUVU ZA HOJA: Sababu za Kiswahili kupendelewa dhidi ya...

WIKI YA LUGHA ZA KIAFRIKA: Tuadhimishe wiki hii ya lugha za...

T L