• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 1:50 PM
Umoja na KPA zashinda kwenye pambano la primia

Umoja na KPA zashinda kwenye pambano la primia

NA PATRICK KILAVUKA

Kocha wa timu ya kikapu ya Umoja Steve Omondi alisema alitumia mbinu ya ulinzi dhabiti na mchezo wa kasi kufunga vikapu hali ambayo ilitumbukiza nyongo matumaini ya wapinzani KU Pirates kwa alama 62-49. 

Hii ilikuwa katika Pambano la Ligi ya Kikapu ya Primia (KBF) ambayo iliandaliwa uwanjani UoN, Nairobi, wikendi. Mwanakikapu bora Dolph Benedict wa Umoja alizoa alama 18 ilhali Pirates walivumishwa na Collins Sudi aliyepachika alama 12.

Katika mchuano mwingine wa upande wa akinadada wa Ligi hiyo,  KPA iliishinda Eagles Wings  57-26. Madina Akot aliiweka KPA kifua mbele kwa alama 12 ilhali Winnie Wafula aliinua Wings kwa kuzoa pointi 10.

Kocha wa  KPA  Antony Ojukwu ambaye ameshinda mara 13 akiwa mikobani mwa timu hii, alisema waliweka ulinzi, kutumia nafasi walizopata vyema na kuzoa mpira  ambayo wapinzani walizipoteza na kujaza alama.

Naye nahodha KPA Vilima Achieng alikariri kwamba wachezaji wao walicheza kama timu, kutumia uzoefu na kujituma hali ambayo ilizaa matunda zaidi. Na katika Ligi ya Mpira wa Kikapu Daraja ya Pili, NEBULAS ilizoa alama  57 -56 dhid ya NEOSASA.

Timu ya mpira wa kikapu ya UMOJA ( Jezi ya kijivu) ikichezea dhidi ya KU Pirates (Jezi ya nyeupe) ambapo zilitoka 62 -29…PICHA/PATRICK KILAVUKA

Mfungaji wa alama nyingi wa NEBULAS alikuwa Clarence Atingo 17 ilhali mchezaji aliyeibuka na alama bora upande wa NEOSASA  alikuwa  Michael Shimechero alizoa pointi 15.Aidha, mchauno mwingine kati ya MAB walipata ushindi 63-43 mbele ya NEBULAS. Aliyeiweka MAB kifua mbele alikuwa Derrick Owino aliyepachika alama 13 naye Kenneth Salo aliipa matumaini timu ya NEBULAS kwa kuizolea alama 14.

MAB (Jezi nyeusi) ikichezea dhidi ya NEBULAS ( Jezi nyekundu) ambapo zilitoka 63-43…PICHA/PATRICK KILAVUKA

 

  • Tags

You can share this post!

Wafanyabiashara walia ushuru ghali wamnyonga raia

Makala ya msanii wa nyimbo za injili Mary Njuguna