• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 AM
Ureno kuvaana na Ujerumani kwenye fainali za Euro U-21

Ureno kuvaana na Ujerumani kwenye fainali za Euro U-21

Na MASHIRIKA

URENO walifunga bao mwishoni mwa kipindi cha pili na kubandua mabingwa watetezi Uhispania kwenye kampeni za kuwania taji la Euro kwa chipukizi wasiozidi umri wa miaka 21.

Ushindi huo wa Ureno uliwakatia tiketi ya kuvaana na Ujerumani kwenye fainali ambayo sasa itasakatwa Juni 6, 2021.

Bao la pekee ambalo Ureno walifunga katika mchuano uliowakutanisha na Uhispania lilitokana na krosi ya Fabio Vieira aliyemzidi nguvu beki Jorge Cuenca.

Ujerumani ambao ni mabingwa mara mbili wa Euro U-21 walifuzu kwa fainali baada ya kuwadengua Uholanzi kwa kichapo cha 2-1 kwenye hatua ya nusu-fainali.

Florian Wirtz alifungia Ujerumani mabao mawili chini ya dakika nane za kipindi cha kwanza kabla ya Perr Schuurs kuwafutia Uholanzi machozi.

Ureno ambao wanajivunia huduma za nyoya Vitinha wa Wolves pamoja na beki Diogo Dalot wa Manchester United, wanapania kutia kibindoni taji la Euro U-21 kwa mara ya kwanza baada ya kuzidiwa maarifa kwenye fainali ya 1994 na 2015.

Kubanduliwa kwa Uhispania kuliwanyima fursa ya kutia kapuni taji la Euro-21 kwa mara sita. Sawa na Uhispania, Italia pia wametawazwa wafalme wa kipute hicho mara tano.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Polisi watibua mkutano wa wanachama wa UDA Pwani

WASONGA: Upimaji corona Kisumu uanzishwe mara moja!