• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 4:25 PM
USHAIRI WENU: Kazi nitazochapa

USHAIRI WENU: Kazi nitazochapa

Na DOTTO RANGIMOTO

YA Rabi kutoka kapa, mjawo ninaogopa,
Kazi nitakazochapa, waja wasije zikopa,
Kisha zisikome hapa, zifike hadi Yuropa.

Nilisema sina pupa, Mungu yupo atanipa,
Iwe nyama ama fupa, kidumu au jipipa,
Neno hili sitatupa, hini dhima nimejipa.

Enda yangu nyapanyapa, taratibu ninadupa,
Nazidi kuchapa lapa, Mola usije nitupa,
Kiapo leo naapa, mpaka sitauchupa.

Tamati kunao papa, Rabi siwezi wakwepa,
Kwa hivi wanavyotapa, dagaa sitanenepa,
Mola naomba wachapa, ili wapate nihepa.

DOTTO RANGIMOTO
‘Jini Kinyonga’
Morogoro

You can share this post!

Presha Tottenham Hotspur na Arsenal zikionana

USHAIRI WENU JUMAMOSI, MACHI 2, 2019

adminleo