• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Uteuzi mwenyekiti IEBC, makamishna sita kuendelea

Uteuzi mwenyekiti IEBC, makamishna sita kuendelea

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA kuu imekataa kusitisha zoezi la kuteua mwenyekiti mpya na wanachama sita wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC).

Lakini Jaji Mugure Thande aliratibisha kesi hiyo iliyoshtakiwa na Seneta wa Busia Okiya Omutatah kuwa ya dharura na umuhimu mkuu kwa umma.

Alisema yapasa kusikizwa na kuamuliwa kwa upesi ili zoezi hilo lisikumbwe na kizugumkuti.

Na wakati huo huo, Jaji Thande aliamuru kesi hiyo isikizwe Aprili 14, 2023.

  • Tags

You can share this post!

Atorosha mke wa babake akidai anamfaa

Karen Nyamu ‘ashambuliwa’ na binamuye Samidoh

T L