Na RICHARD MUNGUTI
MAHAKAMA kuu imekataa kusitisha zoezi la kuteua mwenyekiti mpya na wanachama sita wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC).
Lakini Jaji Mugure Thande aliratibisha kesi hiyo iliyoshtakiwa na Seneta wa Busia Okiya Omutatah kuwa ya dharura na umuhimu mkuu kwa umma.
Alisema yapasa kusikizwa na kuamuliwa kwa upesi ili zoezi hilo lisikumbwe na kizugumkuti.
Na wakati huo huo, Jaji Thande aliamuru kesi hiyo isikizwe Aprili 14, 2023.