• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Wema Sepetu achukua hatua ya nadra kwa mwanamke wa kawaida

Wema Sepetu achukua hatua ya nadra kwa mwanamke wa kawaida

NA FRIDAH OKACHI

MWIGIZAJI Wema Sepetu amefanya uamuzi wa kumlea mtoto wa mpenzi wake Whozu na kumkubali kuwa wake.

Anachukua uamuzi huo baada ya kipindi kirefu cha kutafuta mtoto wake bila mafanikio.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram, mwigizaji huyo alipakia video akiwa na mtoto wa msanii Whozu akicheza na kusema kwamba kachukua hatua hiyo ambaye kwa wanawake wengi, ni ya nadra mno.

Wema alisema kuenda mbele, huyo ndiye mwanawe wa kudumu. Haijalishi chochote kitakachotokea.

“Napenda tu kusema kwamba huyu ndiye m-sweet wangu…,” akasema Wema huku akielezea jinsi juhudi zake za kupata mtoto wake mwenyewe hazijafanikiwa.

Wema amemkubali mtoto wa mpenzi wake huyo mia fil mia.

Siku yake ya kusherekea kuzaliwa kwake, kwenye sherehe hiyo, Wema alisimama upande wa mama na kukaa na mtoto huyo, jambo ambalo liiwavutia watu mitandaoni.

Mapema 2023, kwenye mahojiano, Wema alikiri kwamba amekuwa akitafuta suluhu kila pembe ya dunia kuhakikisha anapata mwanawe.

Mojawapo ya suluhu ilikuwa kusafishwa chupa ya uzazi ili kupata mimba lakini juhudi zote zikaishia kutozaa matunda.

Mwigizaji huyo amekuwa akiishi na Whozu tangu mwaka 2023 baada ya miezi michache Whozu kuachana na baby mama wake.

  • Tags

You can share this post!

Gretsa yalia sera ya Kenya Kwanza kuhusu elimu yaumiza vyuo...

El-Nino: Serikali kuwapa fidia wakulima na wafugaji...

T L