• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 8:55 AM
Wilfried Zaha awataka Palace wamwachilie atafute hifadhi mpya kwingineko

Wilfried Zaha awataka Palace wamwachilie atafute hifadhi mpya kwingineko

Na MASHIRIKA

FOWADI Wilfried Zaha amewataka waajiri wake Crystal Palace wamwachilie ajiunge na kikosi kingine kabla ya maandalizi kwa ajili ya kampeni za msimu ujao wa 2021-21 kuanza mnamo Julai 2021.

Zaha, 28, amesisitiza kwamba kubwa zaidi kayika maazimio yake kitaaluma ni kuvalia jezi za kikosi kitakachompa fursa ya kuanza kunyanyua mataji katika mapambano mbalimbali.

Sogora huyo anayelipwa mshahara wa Sh16.8 milioni kwa wiki uwanjani Selhurst Park, angali na miaka miwili pekee kwenye mkataba wake wa sasa na Palace.

Chini ya kocha Roy Hogson aliyeagana na Palace mwishoni mwa msimu wa 2020-21, Zaha alifungia waajiri wake jumla ya mabao 11 na kuchangia mengine mawili kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Zaha nusura aingie kambini mwa Arsenal au Everton mnamo 2018-19 ila mpango huo ukagonga mwamba baada ya Palace kutaka vikosi vilivyokuwa vikiwania maarifa ya sogora huyo raia wa Ivory Coast wakati huo kuweka mezani kima cha Sh14 bilioni ili kumshawishi kubanduka ugani Selhurst Park.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Ubelgiji wakabwa koo na Ugiriki kwenye gozi la kirafiki

Nyumba za kisasa kujengwa Ruiru na Thika