• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:03 AM
Xavi Hernandez arithi mikoba ya Koeman kwa kishindo

Xavi Hernandez arithi mikoba ya Koeman kwa kishindo

CATALONIA, Uhispania

Na MASHIRIKA

MARA tu baada ya kukabidhiwa mikoba ya ukufunzi wa Barcelona, Xavi Hernandez amesema itabidi sheria kadhaa zibuniwe katika juhudi za kubadilisha timu hiyo na kuirejeshea hadhi yake.

“Nilicheza hapa na baadhi ya wachezaji walio kikosini ambao wanaelewa mfumo wetu na mbinu zinazofaa kutumiwa uwanjani. Iwapo hatuna timu ya kucheza mfumo wetu wa kawaida, itabidi tutafute wachezaji kadhaa wa kuuelewa haraka.

”Xavi alisema itabidi wachezaji wake wawe tayari kucheza nafasi tofauti na kuelewa kudhibiti mpira kwa muda mrefu. Vikwazo tunavyobuni si vya kufinya watu, bali ni sheria zitakazochangia mafanikio ya muda mrefu.

Nitajitolea kusaidia wachezaji kibinafsi na kitaaluma. Ninaelewa changanmoto za kuchezea klabu hii, lakini itabidi tuirejeshe katika uzuri wake,” aliongeza.“Nimewasili siku chache zilizopita, lakini itabidi tukae na Rais wa klabu hii kuhusu mambo kadhaa.

Miongoni mwa mambo hayo ni kuingia sokoni na kusajili nyota kadhaa. Tayari kuna wachezaji kadhaa ambao ni wazuri lakini lazima tuelewe jinsi ya kuwapanga kikosini. Messi amenitumia ujumbe wa kunitakia mema, lakini hayuko hapa kutusaidia na mzigo ni kwa wale waliopo kujitahidi,” aliongeza.

“Kuna wachezaji kadhaa chipukizi kama (Ousmane) Dembele ambao wakinolewa vizuri wanaweza kuwa staa uwanjani. (Dembele) ana kila kipaji na tutamsaidia kuimarika zaidi. Pia itabidi tumpe mkataba mpya aendelee kuwa hapa Camp Nou,” alisema.

Akiwa Barcelona, Xavi aliwahi kucheza na Gerard, Busquets, Jordi Alba, Sergi na Marc-Andre ter Stegen ambao wangali kikosini, lakini kiungo huyo mstaafu amesisitiza kwamba watakuwa miongoni mwa wale atakaosukuma wabebe timu.

Kwingineko, Eddie Howe ndiye kocha mkuu wa Newcastle United ambapo atakuwa na klabu hiyo hadi 2024.“Ni furaha tele kujiunga na klabu hii yenye historia kubwa. Ni jambo la kujivunia pamoja na familia yangu kwa jumla,” alisema kocha huyo wa zamani wa AFC Bournemouth mwenye umri wa miaka 43.

You can share this post!

TAHARIRI: Viongozi wasisute ovyo tume ya IEBC

Washukiwa wawili wakamatwa kwa kuiba paipu za maji

T L