• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Yatima asukumwa rumande kuhusu wizi wa Sh2.5 milioni

Yatima asukumwa rumande kuhusu wizi wa Sh2.5 milioni

Mshukiwa wa wizi Adeshara Krishan Bhailal almaarufu Anilkumar Jakharia akiwa kizimbani kwa wizi wa Sh2.5milioni. Picha/ RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

YATIMA anayekesha kwenye barabara za Nairobi alishtakiwa kwa wizi wa Sh2.5milioni kutoka kwa benki.

Adeshara Krishan Bhailal alishtakiwa kwa kuibia benki ya  Guaranty Trust Bank (GT Bank) pesa hizo.

Kiongozi wa mashtaka Bi Sega hakupinga akiachiliwa kwa dhamana lakini wakili wake Bw David Ayuo alishangaza korti kwa sababu ya ufichuzi wake.

“Mteja wangu huyu hana makazi rasmi jijini Nairobi. Alitupwa na familia yake,” Ayuo alimweleza hakimu mkazi Bi Hellen Onkwani.

Bi Onkwani aliambiwa Bhailal “hana wazazi, na jamaa aliokuwa akiishi nao walimfukuza akaanza kuishi kwa barabara za jijini Nairobi.”

“Unamaanisha mshtakiwa hana familia anayoishi nayo baada ya wazazi wake kuaga?” Onkwani alishangaa.

“ Ndio mshtakiwa hana familia. Anategemea wasamaria wema,”  Ayuo akajibu.

Mahakama haikumwonea huruma ila iliamuru azuiliwe katika gereza la viwandani hadi kesi isikizwe na kuamuliwa.

You can share this post!

Wawili wakana kuiba Sh50 milioni hospitali ya Mater

Miguna Miguna arudishwe nchini, mahakama yaamuru

adminleo