• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:55 AM
Zlatan Ibrahimovic atia saini mkataba mpya wa mwaka mmoja kambini mwa AC Milan

Zlatan Ibrahimovic atia saini mkataba mpya wa mwaka mmoja kambini mwa AC Milan

Na MASHIRIKA

KIGOGO Zlatan Ibrahimovic amerefusha muda wa kuhudumu kwake kambini mwa AC Milan ya Italia kwa mkataba wa mwaka mmoja zaidi.

Ina maana kwamba sogora huyo raia wa Uswidi atakuwa bado akivalia jezi za mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) atakapofikisha umri wa miaka 41.

Ibrahimovic ambaye ataadhimisha miaka 41 ya kuzaliwa mnamo Oktoba 2022, alifungia AC Milan mabao manane ligini mnamo 2021-22 na kuongoza kikosi hicho kunyanyua taji la Serie A baada ya kuwapiku wapinzani wao wakuu, Inter Milan.

Nyota huyo alifanyiwa upasuaji wa goti mnamo Mei 2022 na alitarajiwa kusalia mkekani kwa kipindi cha miezi minane.

Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona, Manchester United na Paris Saint-Germain (PSG), alirejea AC Milan mnamo 2020 na akawasaia kuzoa taji la Serie A mnamo 2021-22, kwa mara ya kwanza baada ya miaka 11.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Arsenal waafikiana na Man-City kuhusu uhamisho wa Oleksandr...

Warembo wa Ubelgiji wapepeta Italia na kufuzu kwa...

T L