• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
NTSA kuwapa wenye magari vitabu vya kidijitali kuzima wizi

NTSA kuwapa wenye magari vitabu vya kidijitali kuzima wizi

Na BERNARDINE MUTANU

Mamlaka ya Uchukuzi na Usalama Barabarani (NTSA) imetangaza mipango ya kuanzisha vitabu vya kielektroniki vya umiliki wa magari kwa lengo la kuzima wizi.

Mkurugenzi Mkuu wa NTSA Francis Meja alisema lengo kuu litakuwa ni kuimarisha utoaji wa habari kupitia sajili yake ya kimtandao (TIMS) katika tovuti ya mamlaka hiyo.

“Kwa sasa tunatathmini uwezekano wa kuanzisha vitabu vya kielektroniki vya kumiliki magari ambavyo vinaweza kuthibitishwa kwa njia rahisi katika mfumo wetu, na kuangalia jinsi mfumo huo unaweza kuunganishwa na kampuni za bima ili kujua mtoaji wa bima,” alisema Bw Meja katika taarifa.

Alisema mfumo huo unatoa nafasi kwa benki kukagua magari chini ya bima yake kielektroniki kwa lengo la kupunguza wizi.

Hii ni kutokana na kuwa mfumo huo unatoa nafasi ya benki kupekua habari kwa lengo la kuzuia wezi.

Hata hivyo hakueleza wakati kamili ambapo NTSA itazindua mpango huo. Septemba mwaka jana, wachunguzi walibaini kundi la wezi lililokuwa likitumia vitabu feki vya gari kwa lengo la kufidiwa.

You can share this post!

Mahakama yamwepushia Kipchoge Keino aibu ya ufisadi

Uhuru kuachia Wakenya deni la Sh7 trilioni...

adminleo