• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Schalke 04 wamtimua kocha Wagner baada ya timu kufungwa mabao 11 mechi mbili za ufunguzi wa Bundesliga

Schalke 04 wamtimua kocha Wagner baada ya timu kufungwa mabao 11 mechi mbili za ufunguzi wa Bundesliga

Na MASHIRIKA

KOCHA wa zamani wa Huddersfield, David Wagner ametimuliwa na Schalke 04 baada ya kikosi hicho kinachoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) kupoteza mechi mbili za kwanza za msimu huu wa 2020-21.

Kupigwa kwa Schalke katika michuano hiyo miwili ligini, kunaendeleza rekodi duni ambayo imewashuhudia wakikosa kusajili ushindi katika jumla ya mechi 18 zilizopita tangu mwisho wa muhula wa 2019-20.

Schalke walipondwa 8-0 na mabingwa watetezi Bayern Munich katika mechi ya ufunguzi wa msimu huu kabla ya kupepetwa 3-1 na Werder Bremen mnamo Septemba 26.

Wagner, 48, alijiunga na Schalke mnamo 2019 baada ya kushawishiwa kuagana na Huddersfield aliowanoa kwa zaidi ya miaka mitatu.

Wasaidizi wake Christoph Buhler na Frank Frohling pia wamefurushwa na Schalke uwanjani Veltins Arena.

Haya yamethibitishwa na mkurugenzi wa spoti wa Schalke, Jochen Schneider.

You can share this post!

John Waw sasa kuwanoa makipa wa Sofapaka

ANA KWA ANA: Resipe anazotengeneza ni mwongozo wa kipekee...