Habari za Kitaifa

Mwandani wa Ruto ajiuzulu, asema anataka kuwania urais 2027

Na FATUMA BARIKI January 11th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

NAIBU Mkuu wa Wafanyakazi Ikulu na Mkuu wa Utekelezaji Miradi ya Serikali katika Afisi ya Rais Eliud Owalo amejiuzulu.

Katika chapisho kwenye kurasa zake za mitandaoni, Bw Owalo ambaye amekuwa mshirika wa karibu wa Rais William Ruto kutoka Nyanza anasema anataka kuwania urais, na kwa sababu hiyo, haingewezekana kwake yeye kuendelea kushikilia wadhifa huo.

Bw Owalo ni naibu wa Mkuu wa Wafanyakazi katika Afisi ya Rais Felix Koskei na ni mmoja wa wanasiasa kutoka Nyanza walioanza kufanya kazi na Rais Ruto mapema mno, hata kabla ya aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kushirikiana na Rais kuunda Serikali Jumuishi.

Kujiuzulu huku kunatarajiwa kuibua hisia mseto hasa kuhusiana na muda ambao hatua hii inajiri, na hatima ya uhusiano wake na Rais Ruto na serikali yake.