• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Mwendwa aahidi Harambee Stars donge nono wakiilima Ghana

Mwendwa aahidi Harambee Stars donge nono wakiilima Ghana

Na Geoffrey Anene

RAIS wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Nick Mwendwa ameahidi Harambee Stars “zawadi nono” ikibwaga Black Stars ya Ghana katika mechi ya Kundi F ya kufuzu kushiriki Kombe la Afrika (AFCON) uwanjani Kasarani jijini Nairobi hapo Septemba 8, 2018.

Tofauti na Ghana, ambayo imtangaza wazi kila mchezaji atatia mfukoni Sh504,300 kwa kuchapa Kenya, Mwendwa hajafichua donge ambalo vijana wa kocha Sebastien Migne watapata. Amesema, “FKF ilikuwa na kikao na wachezaji kuzungumzia suala la kuwapa motisha ya kuwatuza wakipata ushindi. Tuliamua zawadi yenyewe isalie kuwa siri, lakini ningependa kuwahakikishia kwamba ni zawadi ya kudondosha mate. FKF itawatunuku na pia mimi nitafanya mifuko yao iwe mizito kwa kuongeza zawadi hiyo.”

Mwezi uliopita wa Agosti, vyombo vya habari nchini Ghana viliripoti kwamba Kamati ya muda inayoendesha soka nchini Ghana inayojumuisha maafisa kutoka mashirikisho la soka duniani na bara Afrika haijabadilisha motisha ya Sh504,300 kwa kila mchezaji wa Black Stars ikicharaza Kenya.

FKF, ambayo inakabiliwa na wakati mgumu kifedha na kesi 12 mahakamani zinazoigharimu zaidi ya Sh100 milioni ikiwa ni pamoja na kutoka kwa makocha wa zamani wa Harambee Stars Adel Amrouche na Bobby Williamson, haitarajiwi hata kidogo kukaribia kitita cha Ghana.

You can share this post!

#KenyaVsGhana: Mashabiki washenzi waonywa vikali

Hatimaye kesi ya Harambee Starlets dhidi ya Equatorial...

adminleo