TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
  • ePaper
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

[email protected]

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Ulevi si kisingizio cha ushahidi kutokubaliwa kortini,...

September 10th, 2026

Mwanamume aambia korti hajuti kukuza bangi baada ya kukosa...

September 8th, 2026

Ida aidhinisha Raila Jnr kugombea ubunge Kibra 2027

August 24th, 2026

Mama mkarimu auawa na aliyempa maji ya kunywa

August 19th, 2026

Habari Za Sasa

Trump adai Iran inakataa kusitisha vita ‘ili...

September 10th, 2026

Mashambulizi mapya ya ujangili yazuka Turkana, Pokot...

September 10th, 2026

Ulevi si kisingizio cha ushahidi kutokubaliwa kortini,...

September 10th, 2026

Mamia ya watu wafurika Homa Bay baada ya uvumi wa dhahabu...

September 10th, 2026

KenyaBuzz

The Dog Stars

After the world's population has been ravaged by a...

BUY TICKET

Mutiny

After witnessing his billionaire boss' murder and being...

BUY TICKET

The End of Oak Street

After a mysterious cosmic event rips Oak Street from...

BUY TICKET

Piano Soiree 5th Edition: Pop, Props & Pixels

Step into the fifth edition of the annual PIANO SOIRÉE...

BUY TICKET

Redsan @ 30

Celebrating 30 Years of Dancehall RoyaltyOn August 29,...

BUY TICKET

Cellobration 2026

🚨 BEEP BEEP 🚨Attention, revelers and music...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Tanzania yaomboleza kifo cha mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir Hassan

September 7th, 2026

Anajuana na kina Sifuna? Kivutha abadili jina la chama, sasa kuwa ‘The Mwananchi Party’

September 3rd, 2026

Mwenye nyumba ya ‘Bikira Maria’ Kisii aibomoa, adai kuchoshwa na mamia ya ‘mahujaji’

September 7th, 2026

Usikose

Trump adai Iran inakataa kusitisha vita ‘ili kumuumiza’ katika uchaguzi wa ‘mid-term’ Novemba

September 10th, 2026

Mashambulizi mapya ya ujangili yazuka Turkana, Pokot Magharibi

September 10th, 2026

Ulevi si kisingizio cha ushahidi kutokubaliwa kortini, mahakama yaamua

September 10th, 2026
Copyright © 2026 Nation Media Group. All rights reserved.