• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
Salah ahifadhi taji la mwanasoka bora Afrika

Salah ahifadhi taji la mwanasoka bora Afrika

Na GEOFFREY ANENE

STRAIKA wa Liverpool na Misri Mohamed Salah ametangazwa mshindi wa Mwanasoka Bora wa Bara Afrika mwaka 2018 Januari 8, 2019 usiku na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF)  jijini Dakar nchini Senegal.

Salah alipigiwa upatu mkubwa kutetea taji lake. Aling’ara sana katika klabu yake ya Liverpool msimu 2017-2018 na kunyaua taji hilo baada ya kuibuka mfungaji bora katika Ligi Kuu ya Uingereza.

Ingawa alianza msimu 2018-2019 vibaya, amepata makali yake na kumweka pazuri kushinda taji hili la kifahari kwa mara ya pili mfululizo.

Alikuwa na mchango mkubwa katika timu yake ya taifa kufuzu kushiriki Kombe la Afrika (AFCON) mwaka 2019, ambalo mwenyeji atafahamika Januari 9 kati ya Misri na Afrika Kusini baada ya Cameroon kupokonywa majukumu hayo kwa kutokuwa tayari.

Salah, 26, anawania taji la mwanasoka bora wa Afrika dhidi ya mshambuliaji mwenza kutoka klabu ya Liverpool, Sadio Mane, na mvamizi wa klabu ya Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang.

Mgabon Aubameyang amefika fainali tano za wachezaji watatu wa mwisho tangu mwaka 2014. Mwaka 2014, Aubameyang alimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya kiungo mbunifu wa Ivory Coast, Yaya Toure.

Alimpiku Toure na kuibuka bingwa mwaka 2015 kabla ya kumaliza wa pili nyuma ya Riyad Mahrez mwaka uliofuata, ambao ulishuhudia Mane akishikilia nafasi ya tatu. Mara hiyo yote nne alikuwa mchezaji wa Borussia Dortmund nchini Uingereza.

Akiwa mchezaji wa Arsenal, Aubameyang alimaliza katika nafasi ya tatu mwaka 2017 nyuma ya mshindi na mvamizi matata Mohamed Salah kutoka Misri na mshambuliaji Mane. Aubameyang, Salah na Mane wamefungia klabu zao mabao 14, 13 na manane ligini msimu huu, mtawalia.

Hafla yenyewe ya kutuza mwanasoka wa mwaka 2018 itaandaliwa katika jumba la mikutano la Abdou Diouf. Kulingana na CAF, wageni 1,250 wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo Marais Macky Sall (Senegal) na George Weah (Liberia) na Rais wa Shirikisho la Soka duniani (FIFA) Gianni Infantino na mwenzake kutoka CAF, Ahmad Ahmad. Mbali na mwanasoka bora mwanamume kutawazwa, CAF pia itatangaza washindi wa vitengo vya mwanasoka bora mwanamke, kocha bora wa mwaka, timu bora ya taifa na kadhalika.

Mwanasoka bora wa mwaka (mwanamume):

Mshindi    Mwaka     Taifa

Mohamed Salah      2017        Misri

Riyad Mahrez  2016        Algeria

Pierre-Emerick Aubameyang  2015        Gabon

Yaya Toure      2014        Ivory Coast

Yaya Toure      2013        Ivory Coast

Yaya Toure      2012        Ivory Coast

Yaya Toure      2011        Ivory Coast

Samuel Eto’o   2010        Cameroon

Didier Drogba  2009        Ivory Coast

Emmanuel Adebayor       2008        Togo

Frederic Kanoute     2007        Mali

Didier Drogba  2006        Ivory Coast

Samuel Eto’oo 2005 Cameroon

Samuel Eto’oo 2004 Cameroon

Samuel Eto’oo 2003 Cameroon

El Hadji Diouf  2002        Senegal

El Hadji Diouf  2001        Senegal

Patrick M’Boma       2000        Cameroon

Nwankwo Kanu       1999        Nigeria

Mustapha Hadji       1998        Morocco

Victor Ikpeba   1997        Nigeria

Nwankwo Kanu       1996        Nigeria

George Weah  1995        Liberia

Emmanuel Amunike        1994        Nigeria

Rashidi Yekini 1993        Nigeria

Abedi Pele       1992        Ghana

You can share this post!

Kimani Ngunjri ajificha baada ya kuzindua ‘Vuguvugu...

Kizimbani kwa kukwepa ushuru wa Sh97 milioni

adminleo