Dondoo

Demu atishia kuroga mpenzi wa zamani kwa kukataa warudiane

Na JOHN MUSYOKI October 8th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MATERI, THARAKA

KIPUSA wa hapa alitisha kumroga mpenzi wake aliyemwacha miezi kadhaa iliyopita iwapo hangerudiana naye au kumrudishia bidhaa alizomnunulia.

Inasemekana demu alipotengana na jamaa, alimsaka mwanamume mwingine wa kumuoa lakini hakufanikiwa kwa kuwa kila aliyemchumbia alimtaja kama mwanamke anayependa kukalia wanaume chapati.

Siku ya kioja, demu alienda kwa jamaa kutaka warudiane au amrudishie runinga, redio na kabati aliyomnunulia wakati walipokuwa katika uhusiano.

“Sitaishi bila mume na uko hapa. Nimerudi tuelewane. Achana na uliye naye mara moja kwa sababu nimerudi sasa,” demu alimwambia jamaa.

Hata hivyo, jamaa alikataa kumruhusu demu huyo kuwa mpenzi wake tena.

“Siwezi kurudiana na wewe na siwezi kukupatia chochote,” jamaa alisema.

“Kama umekataa nitakuroga. Utajua mimi ni moto wa kuotea mbali,” demu alitisha.