• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 9:50 AM
Chipukizi wa Arsenal anayetikisa buyu la asali ya kahaba

Chipukizi wa Arsenal anayetikisa buyu la asali ya kahaba

Na CHRIS ADUNGO

KIUNGO chipukizi wa Arsenal, Joe Willock, 19, sasa ameapa kumvisha mwanamitindo Eglantine Flore Aguila pete ya uchumba baada ya kuonjeshwa asali majuma machache yaliyopita.

Eglantine ambaye ni kahaba maarufu mzaliwa wa Ufaransa, amewahi pia kuwamegea tunda wanasoka Ashley Cole na Mario Balotelli.

Hadi alipomchezesha Willock miereka ya chumbani, Eglantine alikuwa akitoka kimapenzi na mwanamasumbwi Amir Khan, fowadi Saido Berahino wa Stoke City na aliyekuwa kiungo wa Manchester United, Marouane Fellaini.

Katika mahojiano yake na gazeti la The Sun wiki jana, Willock alikiri kupagawishwa na weledi wa mchezo wa Eglantine chumbani na kubwa zaidi katika maazimio yake kwa sasa ni kumfanya kichuna huyo mwenye umri wa miaka 26 kuwa wake wa halali.

Willcok amewahi pia kujirinia asali mzingani mwa mwanadensi maarufu mzawa wa Australia, Dianne Buswell aliyetemana na mchumba wake Anthony Quinlan mwishoni mwa mwaka jana.

Awali, Eglantine alikuwa amepasua mbarika kuhusu uhusiano wake na Willock kupitia mtandao wa Instagram kwa kusisitiza kwamba kwa sasa penzi lake limepata hifadhi salama na ya kudumu moyoni mwa tineja huyo matata wa Arsenal japo ‘hakumfanyia kazi nzuri’ walipovaana kwa mara ya kwanza kimahaba.

Katika ujumbe wake, Eglantine alipakia pia picha alizopigwa kwa pamoja na Willock huku mengi ya mabusu aliyokuwa akilirushiwa na ‘dume’ lake yakiashiria ukubwa wa kiwango cha kukomaa kwa penzi lao.

Kipusa huyo aliungama kwamba alimfungulia Willock buyu lake la asali kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa mwezi jana wakati Arsenal walipowazuru Blackpool kwa mechi ya raundi ya tatu ya Kombe la FA uwanjani Bloomfield Road.

Katika mchuano huo, Willock aliwafungia waajiri wake mabao mawili na kuchangia ushindi wa 3-0 uliowapa Arsenal tiketi ya kuvaana na Manchester United waliowadengua baadaye katika raundi ya nne ya Kombe la FA.

Ungamo la Eglantine lilimweka Willock kwenye ‘kurasa mbovu’ za madaftari ya wachanganuzi wa soka ambao kwa sasa wanahisi kwamba huenda chipukizi huyo akapotoshwa zaidi kimaadili na Eglantine asiyetosheka kirahisi na huduma za chumbani.

Mnamo 2015, Eglantine alikiri kutoridhishwa na mchezo wa aliyekuwa beki wa Chelsea, Cole huku akitetea tukio la tunda lake kudokolewa pia na mvamizi wa sasa wa Olympique Marseille, Mario Balotelli.

You can share this post!

Pogba injini ya Man United

Fred sasa ni kidume kamili, afunga bao la hakika

adminleo