Waandamanaji wakikabiliana na polisi eneo la Meru, huku wakiwasha moto magudurumu barabarani. Picha|David Muchui
JUMATANO, Juni 25, 2025 maafisa wa polisi kukabiliana na ghasia walikabiliwa na kibarua kigumu kutuliza waandamanaji wa kizazi cha Gen Z, waliojitokeza karibu kila kona ya nchi dhidi ya ukatili wa polisi.
Zaidi ya kaunti 20 zilishuhudia machafuko, vijana wakilalamikia dhuluma za maafisa wa usalama.
Idara ya Polisi (NPS) imejipata kwenye kikaango moto hasa kufuatia kifo cha mwalimu na mwanablogu Albert Ojwang’ akiwa kwenye seli ya polisi, tukio la kinyama lililoibua hasira kwa Wakenya.
Gari la polisi likipiga doria Voi, Taita Taveta. Picha|Lucy Mkanyika
Maafisa kadhaa, wakiwemo Mkuu (OCS) wa Kituo cha Polisi cha Nairobi ya Kati, Samson Taalam, na naibu wake Samuel Ng’ang’a, mshukiwa mkuu wa mauaji hayo — Konstebo James Mukhwana, pamoja na raia kadhaa tayari wamekamatwa huku uchunguzi ukiendelea.
Wakiendelea kuzuiliwa, washukiwa hao wamefikishwa mahakamani huku wito ukizidi kutolewa wa kukamatwa kwa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi (Kitengo cha Polisi wa Kawaida), Eliud Lagat, ambaye hivi majuzi alitangaza kujiondoa kwa muda kwenye ofisi ya hadhi ya juu anayoshikilia ili kuruhusu uchunguzi kufanyika.
Kizuizi kuingia jijini Nairobi, eneo la Kasarani. Picha|Sammy Waweru
Lagat, ambaye bado yuko kikosini, ametajwa kuhusika na kifo cha Ojwang’, kwani anadaiwa kuagiza maafisa wa Idara ya Upelelezi wa Jinai na Uhalifu (DCI) kumkamata bloga huyo nyumbani kwake, Kaunti ya Homa Bay.
Taifa Dijitali imekusanya na kuandaa picha za wanahabari wetu, kutoka sehemu mbalimbali za nchi kuonyesha hali na taswira ilivyokuwa:
Gurudumu lililowashwa moto Homa Bay. Picha|George OdiwuorKundi la vijana wakijiandaa kuingia barabarani kushiriki maandamano Embu. Picha|George MuneneMagari eneo la Carwash, Thika Road, Nairobi yakirejea kujiunga na barabara ya kasi baada ya eneo la Kasarani kuwekwa kizuizi dhidi ya kuingia jijini Nairobi. Picha|Sammy WaweruVijana Ol Kalou, Nyandarua wakiandamana. Picha|Waikwa MainaKisii Mjini waandamanaji wakiwa wamewasha magurudumu moto. Picha|Wycliffe NyaberiVijana eneo la Lamu, Kilifi wakishika vibango kuashiria kuchoshwa na ukatili wa polisi. Picha|Kalume KazunguVipande vya risasi vinavyoaminika kutumika na polisi kufyatulia waandamanaji Thika Road, Nairobi. Picha|Nyaboga KiageJijini Nairobi maandamano yakianza asubuhi. Picha|Sammy WaweruVijana eneo la Voi, Taita Taveta wakiwa na vibango. Picha|Lucy MkanyikaJuu ya mzunguko wa Globe, Nairobi vijana wakiingia kwa mpango jijini Nairobi licha ya maafisa wa polisi kutwaa kila kona. Picha|Sammy WaweruNyeri Mjini vijana wakianza maandamano asubuhi. Picha|Mercy MwendeMaafisa wa trafiki eneo la Kasarani wakilinda kizuizi. Picha|Sammy WaweruMojawapo ya maduka yaliyobomolewa na kuporwa bidhaa Jijini Nairobi. Picha|Kevin CheruiyotMaafisa wa kukabiliana na ghasia eneo la Kasarani wakizuia matatu dhidi ya kuelekea Jijini Nairobi. Picha|Sammy WaweruWanahabari Kisii wakijaribu kunasa picha na video ya polisi wakirushia waandamanaji gesi ya vitoza machozi. Picha|Wycliffe NyaberiMagari machache yakihudumu Thika Super Highway, kinyume na inavyoshuhudiwa siku zingine. Picha|Sammy WaweruAfisa wa polisi Kitengela, Kajiado akikabiliana na waandamanaji. Picha|Stanley NgothoEneo la Ngara, Nairobi ambapo asubuhi matatu yalikuwa yakifika. Magari ya huduma za umma yalizuiwa dhidi ya kuingia katika kitovu cha jiji la Nairobi. Picha|Sammy WaweruHussein Khalid, Mkurugenzi Mkuu wa Haki Africa, akizungumza nje ya jengo la Nation, Nairobi. Picha|Sammy Waweru