• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
Jela ambapo wafungwa huondoka kila siku kwenda kusaka riziki

Jela ambapo wafungwa huondoka kila siku kwenda kusaka riziki

MASHIRIKA Na PETER MBURU

KATIKA jela ya Sanganer katika Jiji la Jaipur, India kuna mazingira ya aina yake kwani japo wahalifu hufungwa humo, hawapewi chakula.

Kutokana na hilo, inawabidi wafungwa kila siku kwenda kutafuta kazi za vibarua ili kupata riziki, nje ya gereza.

Jela hiyo, ambao iko taifa la Rajasthan, magharibi mwa India haina kuta, vizuizi wala walinzi kwenye lango. Wafungwa huhimizwa kwenda jijini kila siku kujitafutia riziki.

Ilianzishwa miaka ya 1950 na kila wakati ina wafungwa 450. Ni moja ya taasisi nyingine za aina hiyo takriban 30 katika taifa hilo la Rajasthan.

Watu waliohukumiwa kwa makosa makubwa kama kuua, wizi wa mabavu na mengine hupata makao humo.

Taifa hilo limekuwa likizidisha juhudi za kuwepo kwa magereza wazi, kampeni inayoongozwa na Bi Smita Chakraburtty, akitaka iwe kawaida kote India.

Bi Chakraburtty amefikisha kesi katika mahakama ya juu India, ambapo anataka mataifa madogo tofauti ndani ya nchi pana ya India kuanzisha jela za aina hiyo.

Tayari mataifa mengine manne huko India yameanza kutekeleza mfumo huo wa magereza, kwani mwaka uliopita yalifungua jela za aina hiyo.

“Muundo wa utoaji haki katika sheria za kijinai ni wa kushughulikia vitendo lakini mtendaji huwa haangaziwi,” akasema Smita.

Hakuna walinzi katika jela hizo na kila anayetaka kutembea humo ndani huwa yuko huru.

Wengi wa walio katika jela ya Sanganer ni wale waliofungwa kwa makosa ya mauaji. Wafungwa katika jela hiyo huona maisha yakiwa rahisi na kila wakati wamefurahi.

Lakini kabla ya kupelekwa katika jela hiyo, wote sharti wawe wamehudumia thuluthi mbili za muda wa kifungo katika jela ya kudhibitiwa, wakiona jela hiyo ya kisasa kuwa uhuru kabisa.

Kukatalia ndani

Tangu kuundwa kwa jela hiyo, serikali inasemekana kuwa na wakati mgumu wakati vifungo vya wafungwa vinapokamilika kwani wengine wao wanakatalia humo.

Katika nyakati fulani, serikali inalazimika kuwafukuza wafungwa kutoka gerezani kwa lazima, kwani wanakataa wanapoona kuwa kuna shule na mazingira mazuri humo ndani.

Wafungwa hao huendesha maisha kikawaida humo ndani kwani wanaweza kununua vitu kama simu, pikipiki na runinga wanapofanya kazi.

Aidha, hawavai sare yoyote ya jela na wanaishi kwa vikundi vidogo. Hata hivyo, jela haiwapi kitu kingine kama chakula, pesa wala maji na hivyo inawabidi kuondoka kutafuta kazi.

Ni kwa sababu hii ndipo kila siku utawapata wengi wao wakiondoka kutoka jela hiyo kwenda kutafuta riziki, japo ni wafungwa.

Wanaume waliofungwa kwa mauaji hufanya kazi za ulinzi, wa viwanda na vibarua vingine vya kila siku.

Wanaadhibiana

Sheria ya pekee ni kuwa wafungwa hao sharti kila siku jioni waangaliwe ikiwa wako wote. Ni mfungwa ambaye huendesha zoezi hili. Kwa kawaida, ni wafungwa wenyewe ambao hujiongoza na kuadhibiana panapokuwa na makosa.

Mfungwa akijaribu kutoroka kutoka jela hii anahatarisha kurudishwa katika jela ya kufungiwa ndani.

Wafungwa wengi, hata hivyo, bado huadhiriwa na hali kuwa watu wengi wa kawaida huhusisha mazingira wanamoishi ya jela kuwa yasiyo mazuri na hivyo huwaona kama watu wasiokuwa wa kuaminika. Baadhi ya watu huwanyima kazi wanapotoa vitambulisho vyao vya jela.

Lakini kwa wanawake, wengi wao wamesema kuwa angalau mazingira hayo ya jela hiyo yamewafaa kwa kuwawezesha kukutana na wanaume ambao wamewapenda.

Wanawake wengi walikiri kuwa wamepata waume ambao wameanzisha familia nao, hivyo wakijihisi wakamilifu.

You can share this post!

LEUSHADORN LUBANGA: Afichua kutamaushwa na waigizaji wa...

Michael Jackson alipenda kujichua akitumia Vaseline –...

adminleo