• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 11:55 AM
Kaunti 10 zenye bidii ya kuiletea Kenya mapato

Kaunti 10 zenye bidii ya kuiletea Kenya mapato

Na BERNARDINE MUTANU

Kaunti ya Nairobi ndiyo iliyoipa Kenya mapato mengi zaidi ikilinganishwa na kaunti zingine.

Kulingana na ripoti ya hivi punde ya Shirika la Kitaifa la Takwimu (KNBS), Nairobi ilitoa asilimia 21.7 ya mapato yote katika muda wa miaka mitano.

Uchunguzi wa kwanza kuhusu mapato ya jumla ya kaunti (GCP) 2019 ulionyesha kuwa kaunti zingine zilizoipa Kenya mapato zaidi ni Nakuru, Kiambu na Mombasa.

Uchunguzi huo ulihusu thamani ya bidhaa na huduma zilizotolewa katika kila kaunti nchini.

Kaunti zingine zilizo katika nafasi ya 10 bora ni Nakuru (asilimia 6.1), Kiambu (asilimia 5.5), Mombasa (asilimia 4.7), Machakos (asilimia 3.2), Meru (asilimia 2.9) na Kisumu (asilimia 2.9),Nyandarua (asilimia 2.6) Kakamega (asilimia 2.4) na Uasin-Gishu (asilimia 2.3).

Isiolo ilitoa asilimia 0.2 ilhali Samburu ilitoa asilimia 0.3 na kushikilia mkia katika ripoti hiyo inayoonyesha kiwango cha mapato ya serikali kutoka katika maeneo ya kaunti.

You can share this post!

Mfumo wa kidijitali wa maegesho JKIA wasimamishwa

Polisi watibua uwezekano wa machafuko kuhusu ardhi...

adminleo