Shangazi Akujibu
Mume wangu amezamia majukwaa ya kusaka wapenzi mitandaoni!
SWALI: Kwako shangazi. Nilishtuka kumkuta mume wangu akiwa na akaunti ya kutafuta wachumba mtandaoni. Anasema ilikuwa mzaha tu. Je, nimwamini?
Jibu: “Mzaha” wa kutafuta wachumba si mzaha, ni usaliti. Kama kweli hana kitu cha kuficha, aifute mbele yako. Ukiona anasitasita, jua moyo wake una wavu wa sumu.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO