Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Mume ataka kunitenga katika utunzaji wa pesa za kodi tukijenga ploti
PICHA | HISANI
SWALI: Tunapanga kujenga nyumba ya kukodisha lakini mume wangu anasisitiza pesa zote ziwekwe kwa jina lake. Je, ni sawa?
Jibu: Ikiwa ni mali ya ndoa, haina haja kuandika jina la mtu mmoja. Shirikianeni kwa uwazi na muweke kila kitu kwa haki kwa manufaa yenu wawili. Kuna wale huchagua kukubaliana wafungue akaunti za pamoja ili uwazi upatikane. Mnaweza kufanya uamuzi wenu.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO