Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Anatumia mwanamke mwingine pesa zake
Noti za Sh1,000 pesa za Kenya. PICHA | MAKTABA
SWALI: Shikamoo shangazi. Mume wangu anadaiwa na kila mtu, lakini amekuwa akituma pesa kwa mwanamke fulani kila mwisho wa mwezi. Je, hili linafaa kunitia wasiwasi?
Jibu: Ni kawaida kuanza kuwa na wasiwasi ukiona dalili kama hizo. Uwazi na mazungumzo ni muhimu. Muulize kwa utulivu ni kwa nini anatuma pesa kwa mwanamke huyo. Hii itakusaidia kuelewa uhusiano wake na mwanadada huyo.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO