Habari

Uchaguzi wa kujaza kiti cha Ng’eno kuhitaji Sh59 milioni

Na SAMWEL OWINO March 11th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

UCHAGUZI mdogo wa eneo bunge la Emurua Dikir utagharimu walipa ushuru takriban Sh59 milioni, kulingana na stakabadhi zilizowasilishwa bungeni na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

Tume hiyo imeiomba Bunge la Kitaifa kuitengea Sh59,375,491 katika bajeti ya ziada ya pili ya mwaka wa fedha wa 2025/26 ili kufanikisha uchaguzi huo.

Wakati  huo huo, ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya, utovu wa nidhamu na dhuluma za kingono dhidi ya watoto shuleni umesababisha wabunge kushinikiza mpango wa ushauri nasaha kuwa wa lazima katika shule zote za msingi na sekondari.

Wabunge wanahofia kuongezeka kwa visa vya watoto kudhulumiwa kingono, ikiwemo kuuawa na watu walio karibu nao.