Habari za Kaunti

Kingi: PAA haijavunjwa, lakini haitakuwa na wagombeaji 2027

Na WINNIE ATIENO March 18th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

CHAMA cha Pamoja African Alliance (PAA) hakijavunjwa, Spika wa Seneti Amason Kingi amefafanua.

Hata hivyo, chama hicho hakitawasilisha wagombeaji katika Uchaguzi Mkuu wa 2027.

Badala yake, alisema chama hicho kitaunga mkono wagombea wa chama cha UDA, huku wanasiasa ambao wangewania nyadhifa kupitia PAA sasa wakitarajiwa kuwania kupitia UDA.

Spika Kingi alifafanua kuwa msimamo wa chama hicho ni tofauti na ripoti za Alhamisi katika ukurasa huu kwamba chama hicho kimekubali kumezwa na UDA ya Rais William Ruto.

Kwa mujibu wa Spika Kingi ambaye alihudumu kama gavana wa Kilifi kwa mihula miwili, PAA bado ipo kisheria kama chama cha kisiasa, lakini kimeamua kimkakati kutowasilisha wagombeaji wake katika uchaguzi ujao na badala yake kushirikiana na UDA.

PAA ni chama tanzu cha Muungano wa Kenya Kwanza unaoleta pamoja UDA na vyama vingine.