Michezo

Mshonaji wa sare apangia makazi, uwekezaji baada ya ushindi wa SportPesa midweek Jackpot

Na CECIL ODONGO April 5th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

CAROLINE Mmbone ambaye ni mshonaji wa sare za shule sasa analenga kukumbatia uwekezaji wa kupanua biashara zake na kununua shamba katika Kaunti ya Kajiado.

Mwanadada huyo alishinda Sh9.5 milioni kwenye droo ya SportPesa midweek Jackpot, pesa ambazo sasa analenga kutumia kuhakikisha ana makazi mazuri.

Bi Mmbone alijifunza kucheza kamari ya SportPesa kutoka kwa wanawe watano wa kiume ambao walikuwa wakiwekeza pesa kidogo kidogo na kupata ushindi.

Ingawa alikuwa akishiriki ubashiri kwa kutumia pesa kidogo, hakufaulu kuwahi ushindi hata mara moja kabla ya huu uliompa Sh9.5 milioni.

“Sikuamini kile ambacho niliona kwenye akaunti yangu. Nilifurahi sana baada ya kuona nimeshinda,” akasema.

Mmbone alisema analenga kutumia hela hizo kujenga nyumba ili kumpunguzia gharama ya kulipa kodi na pia amakinike zaidi katika kuimarisha biashara zake.

“Nawaambia wale ambao hubashiri mechi hasa vijana wafanye hivyo kwa hekima. Kuna nafasi lakini hekima na heshima ni muhimu zaidi,” akaongeza.

Ilikuwa ni furaha riboribo nyumbani kwake baada ya kupata ujumbe ulioonyesha ameshinda hela hizo na hata kuangalia masalio yake kwenye akaunti yake ya SportPesa.

Mmbone alisema ana mume ambayo watashauriana jinsi ya kutumia hela hizo akimsifu kuwa amekuwa nguzo ya familia yao.

Kando na Mmbone, wengine ambao waliwahi ushindi baada ya kubashiri mechi vilivyo walikuwa Stanley Kiptoo na Joseph Lagho.