Dondoo

Polo abaki kigugumizi mademu ‘aliowacheza’ walipomkabili aoe mmoja wao

Na MWANDISHI WETU July 2nd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KOIWA, Bomet:

POLO alibaki ulimi nje mademu wake wawili walipomtembelea pamoja na mmoja wao kumtaka amvishe pete mwenzake.

Vipusa hawa walipojua kuwa wanatoka na jamaa mmoja waliamua kutafuta suluhu badala ya kupigana kwani ni marafiki.

“Tumejua vile unatufanyia na nimeamua kujaribu bahati kwingine bila chuki kwako ama huyu mrembo. Ni vyema kama utamuoa huyu shogangu,” banati alisema.

Inasemekana polo alipatwa na kigugumizi na akashindwa kutoa jawabu waziwazi lakini hatimaye akaahidi kufanya hivyo.

Baadaye jombi aliarifu wandani wake kuwa aliyejitoa ndiye alikuwa barafu wa moyo wake na akajuta kuramba asali huku na kule.