Ni mguu niponye kwa buda aliyesakwa na mbunge kwa kutumia jina lake vibaya
KULIZUKA kioja mjini hapa juzi baada ya polo mmoja kuchana mbuga kumhepa mheshimiwa aliyekuwa akimtafuta kwa hasira.
Inadaiwa polo huyo alikuwa akijigamba kwa marafiki kuwa ana ushawishi mkubwa kwa mwanasiasa huyo, lakini mambo yaligeuka baada madai kuwa alikiuka makubaliano yao.
Mbunge alipowasili ghafla katika eneo hili juzi, polo alitokomea mbio bila hata kugeuka nyuma.
Katika purukushani hizo, aliacha kiatu kimoja njiani huku walioshuhudia wakipasuka kwa vicheko.
Baadhi ya wakazi walitania kwamba “miguu ndiyo ilimshauri kuliko akili.”
Jamaa alijitokeza baada ya mheshimiwa kuondoka kuokota kiatu chake alipohakikishiwa hali ilikuwa shwari.