Dondoo

Usivunje ndoa yako sababu ya michepuko, wanaume wote ni mafisi, kidosho ashauriwa

Na MWANDISHI WETU August 18th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

TALA, Kangundo:

DEMU wa hapa, alishauriwa na wenzake asivunje ndoa baada ya kugungua mumewe anachepuka, wakisema hatapata mwanamume asiye na kimada.

Mwanadada huyo alishindwa kuvumilia baada ya kubaini kuwa mumewe alikuwa akichati na warembo chungu nzima kwenye simu.

Inasemekana kipusa huyo, ambaye amekuwa kwenye ndoa kwa miaka mitano, hakuwa amepekua simu ya mumewe hadi juzi jamaa alipoisahau nyumbani.

Kwa udadisi, kidosho aliamua kuichunguza na kupata jumbe za kimahaba zilizokuwa zikitumwa kwa wanawake wengine.

Akijawa na hasira, alitishia kufunga virago na kuondoka, akisema amechoka kuvumilia michepuko ya mumewe.

Hata hivyo, baadhi ya wenzake majirani walimsihi asikimbilie kuvunja ndoa wakisema wanaume wamezoea kuwa na vimada.

“Mrembo, usihepe ndoa kwa sababu ya vimada. Wanaume ni mafisi, lakini bora umjue wako kuliko kuanza upya,” walimshauri.