Samia aachia uongozi makamu wake Ndejembi akienda kuomboleza mumewe
MAKAMU wa Rais Deogratius Ndejembi na Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba wanatarajiwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha shughuli za serikali Tanzania zinaendelea bila kusita huku Rais Samia Suluhu Hassan akiomboleza kifo cha mumewe, Hafidh Ameir Hassan.
Bw Ameir alifariki Jumatatu akipokea matibabu ya ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Emilio Mzena, Zanzibar.
Alizikwa siku hiyo hiyo katika kijiji cha Kizimkazi, Zanzibar, kwa mujibu wa mila za Kiislamu.
Makamu wa Rais Ndejembi, ambaye aliapishwa Agosti 29 baada ya Emmanuel Nchimbi kuondoka madarakani, ndiye anayeshikilia nafasi ya pili kwa mamlaka katika nchi hiyo.
Wakati huu wa maombolezo, Ndejembi anatarajiwa kumsaidia Rais katika kutekeleza majukumu ya serikali, huku Waziri Mkuu Nchemba akiendelea kuratibu shughuli za kila siku za serikali.
Licha ya kuomboleza kifo cha mumewe hakiondoi mamlaka yake ya kikatiba kama Rais.