WHO imesema Ebola bado ni changamoto na inahitaji rasilimali nyingi.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus,alisema Jumatano kwamba hadi kila maambukizi yatakapobainika na kukatizwa, ugonjwa huo utaendelea kuwa hatari DRC, nchi jirani na eneo lote.

Idadi ya waliofariki kutokana na mkurupuko huo imevuka 3,000, kwa mujibu wa takwimu za serikali, huku ugonjwa huo ukiendelea kuenea kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.

Mkurupuko huo, unaosababishwa na aina ya kirusi cha Ebola cha bundibugyo, sasa ndio mkubwa na wenye vifo vingi zaidi katika historia ya DRC na imezidi mkurupuko uliotokea mnamo na 2018–2020.

Tedros alisema vifo vingi vimetokea miongoni mwa watu ambao hawakuwa kwenye orodha ya waliokuwa wamewasiliana na wagonjwa, hali inayoashiria kuwepo kwa maambukizi mengi ambayo hayajulikani.

Alisema mazishi yasiyofanywa kwa njia salama pia yanaendelea kuchangia kuenea kwa virusi hivyo.

WHO imeomba kuongezwa kwa fedha za mpango wa kukabiliana na Ebola unaoongozwa na serikali ya Congo, unaohitaji dola bilioni 1.3 (Sh168 bilioni).

WHO imetuma tani 320 za vifaa na kuongeza uwezo wa vipimo hadi 3,000 kwa siku, lakini inahitaji fedha zaidi kuongeza vitanda katika vituo vya matibabu.