• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 11:05 AM
Afikishwa kortini bila viatu kwa kuiba mtoto

Afikishwa kortini bila viatu kwa kuiba mtoto

Bi Edinah Kerubo Mabuka alipofikishwa kortini kwa makossa ya kumwiba mtoto wa wiki tatu. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAMKE anayeshukiwa kumwiba mtoto wa wiki tatu Jumatano alifikishwa kortini jijini Nairobi bila viatu.

Hakimu mwandamizi Kennedy Cheruiyot aliamuru Edinah Kerubo Makuba azuiliwe katika kituo cha polisi cha Kilimani kuwasaidia polisi kuwafichua wanachama wa genge linalowaiba watoto.

Afisa anayechunguza kesi hiyo aliambia korti mahojiano aliyofanya yamedhihirisha kuwa mshukiwa huyu ni mshirika wa kundi la kuwaiba watoto linaloendesha biashara jijini Nairobi na maeneo mengine.

Koplo Emmanuel Kiptoo alisema mshukiwa huyo yuko na taarifa ambazo zitasaidia polisi kuwafikia  washukiwa zaidi.

Bw Cheruiyot aliamuru Kerubo azuiliwe kwa siku tano.

Kerubo alikiri huyo ndiye alikuwa mtoto wake wa kwanza kumwiba na alikuwa anatazamia kumrudishia mama yake.

Atarudishwa kortini Jumatatu kushtakiwa.

You can share this post!

Mtanzania anaswa JKIA akiwa na dhahabu ya Sh100 milioni

Miguna Miguna: Raila ndiye aliniambia Jubilee ilimpa Magaya...

adminleo