• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 3:03 PM
Mwanamume ashtakiwa kujifanya Jaji Ibrahim

Mwanamume ashtakiwa kujifanya Jaji Ibrahim

Na RICHARD MUNGUTI na PHYLIS MUSASIA

MWANAUME alishtakiwa Ijumaa kwa kujifanya Jaji Mohammed Ibrahim wa Mahakama ya Juu.

Henry Antony Wasike alikanusha shtaka la kuandikisha laini ya simu katika kampuni ya Safaricom akijifanya kuwa Jaji Ibrahim.

Shtaka dhidi ya Bw Wasike lilisema mnamo Februari 26, 2019, mwendo wa saa tatu na dakika 14 asubuhi alisajili laini ya simu ya kampuni ya Safaricom akitumia jina la Jaji Mohammed Ibrahim wa Mahakama ya Juu.

Ilidaiwa kwamba mshtakiwa alifanya hivyo akiwa na nia ya kutumia laini hiyo kutenda uhalifu.

Bw Wasike ambaye hakuwa amewakilishwa na wakili aliomba Hakimu Mkuu Bw Francis Andayi amwachilie kwa dhamana.

“Ninaomba mahakama iniachilie kwa dhamana wa sababu hadi sasa sina hatia na niko hapa kwa madai tu,” mshtakiwa alimsihi Bw Andayi.

Kiongozi wa mashtaka Bi Kajuju Kirimi hakupinga kuachiliwa kwa mshtakiwa kwa dhamana.

“Dhamana ni haki ya kila mshukiwa kwa mujibu wa kifungu nambari 49 cha katiba,” alisema Bi Kirimi.

Bw Andayi aliamuru mshtakiwa aachiliwe kwa dhamana ya Sh50,000 pesa tasilimu hadi Mei 6, 2019.

Watu watatu wameorodheshwa kufika mahakamani kutoa ushahidi.

Mahakama iliamuru kiongozi wa mashtaka ampe mshtakiwa nakala za ushahidi ndipo aandae ushahidi wake.

Nakala za ushahidi

Mahakama iliamuru kiongozi wa mashtaka ampe mshtakiwa nakala za ushahidi ndipo aandae ushahidi wake.

Kesi itatajwa Mei 29 ili upande wa mashtaka uthibitishe ikiwa umempa mshtakiwa nakala za mashahidi kisha maagizo zaidi yatolewe ikiwa ni pamoja na kutengewa tarehe ya kusikilizwa.

Kwingineko mjini Nakuru, mwanamume mwenye umri wa miaka 70 alikanusha kulaghai mfanyabiashara Sh680,000 akidai angemuuzia ploti.

Micheal Ndungu Muriuki alidaiwa kumtapeli Bi Priscilla Wambugu pesa hizo eneo la Kabatini Kaunti ya Nakuru.

Kesi itasikilizwa Mei 24, 2019.

You can share this post!

Wizara yasaka Sh6 bilioni kukabili njaa

Kariobangi Sharks waanza vizuri safari ya kutetea taji la...

adminleo