• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Taabani kwa kukosa kulipia ngozi ushuru

Taabani kwa kukosa kulipia ngozi ushuru

Godfrey Bosire akiwa kizimbani aliposhtakiwa kwa uuzaji ng’ambo zaidi ya kilo milioni 3 za ngozi za ng’ombe na kukwepa kulipa mamlaka ya ushuru nchini (KRA) Sh204 milioni. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

MFANYABIASHARA alishtakiwa Jumatatu kwa kuuza ngozi za ng’ombe kilo 3,862,264  ng’ambo na kukwepa kulipa serikali ada ya forodha iliyopelekea serikali kupoteza ushuru wa Sh204 milioni.

Bw Godfrey Bosire alikanusha shtaka hilo mbele ya hakimu mkuu katika mahakama ya miliamni Bw Francis Andayi.

Kiongozi wa mashtaka Bw Solomon Naulikha aliomba kesi hiyo dhidi ya Bw Bosire itajwe Jumanne kwa lengo la kuiunganisha na  nyingine ambapo Bi Clare Marisiana Odimwa alishtakiwa kwa kosa kilo hilo.

Bw Naulikha alisema nakala za mashahidi katika kesi hiyo ziko tayari na kuwa Bw Bosire anaweza kuzipokea aandae tetezi zake.

Kiongozi huyo wa mashtaka alisema kuwa katika kesi dhidi ya Odimwa mahakama ilimwachilia kwa dhamana ya Sh500,000 na mdhamini mmoja wa kiasi sawa na hicho.

Pia alisema mshtakiwa huyo  alipewa dhamana ya pesa tasilimu Sh100,000.

Wakati huo huo Bi Margret Awino Magero alishtakiwa kwa kupokea sabuni na mafuta ya kupikia za thamani ya Sh 17 milioni kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa Mabw Jeremiah Kiplangat Kendagor na Bw  Lukas  Oketch Mandagi Desemba 2016.

Alikanusha mashtaka na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 pesa taslimu.

You can share this post!

Waliovuta bangi ili wakanengue viuno kwa shoo ya Freddie...

Hakimu aamuru anayedaiwa kuiba kioo apelekwe hospitalini...

adminleo