• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 3:53 PM
Polo agutusha kijiji kuficha ng’ombe kwa kimada

Polo agutusha kijiji kuficha ng’ombe kwa kimada

Na TOBBIE WEKESA

EKERENYO, NYAMIRA

KALAMENI mmoja aliwashangaza wenyeji wa hapa alipoamua kuwahamisha ng’ombe wake hadi kwa mpango wake wa kando.

Inasemekana katika tukio hilo lililowaacha wengi vinywa wazi, polo alichukua hatua hiyo akidai kwamba mke wake haaminiki kabisa.

Duru zinasema kalameni alianza kumshuku mkewe mashemeji wake walipoanza kwenda kwake bila kumfahamisha.

“Tangu ninunue hawa ng’ombe, ndugu zako wamekuwa wakija hapa kila wakati. Mbona huniambii wakija na sababu yao ya kuja,” polo alimkaripia mkewe.

Kulingana na mdokezi, sababu aliyoitoa mkewe haikumridhisha polo. “Nahofia sana ng’ombe wangu. Sioni hawa watu wako wakiwa na nia njema,” polo alidai huku akielekea zizini na kuwafungulia ng’ombe.

“Naona leo umewafungulia mifugo mapema sana. Kwani unawepeleka malishoni umbali gani na hii mvua?” mkewe alimuuliza kalameni. Inasemekana polo alimkanya mkewe kuingilia mambo ayafanyayo.

“Achana na mali yangu kabisa. Ikiwa ni malishoni nawapeleka haikuhusu. Ni mimi niliwanunua,” kalameni alimkaripia mkewe.

Maneno ya polo yalimshtua kipusa. “Nahofia sana ng’ombe wangu kuchukuliwa na watu wa kwenu. Heri niwafiche mahali salama,” polo alimueleza mkewe.

Alipotaka kujua mahali salama alikodai kuwapeleka ng’ombe, polo alimueleza mkewe kwamba alikuwa akiwapeleka kwa mwenzake.

“Hii mali yangu naipeleka kwa mwanamke mwenzako ambaye hana njama na watu wao kama wewe. Acha maswali mengi,” kalameni alimueleza mkewe huku akienda.

Duru zinasema baada ya kuwafungulia ng’ombe wake, polo alianza safari kuelekea kwa mpango wa kando katika kijiji jirani kuwaficha humo.

…WAZO BONZO….

You can share this post!

Mabilionea nchini waongezeka licha ya serikali kulia haina...

Janga la bidhaa feki linavyoilemaza Kenya kiuchumi na kiafya

adminleo