• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 6:47 AM
UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Sifa za mkufunzi, mwanagenzi katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Sifa za mkufunzi, mwanagenzi katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili

Na MARY WANGARI

ILI kufanikisha mchakato wa ufundishaji wa lugha ni muhimu kwa mkufunzi kudhihirisha sifa zifuatazo:

i. mkufunzi anapaswa kuwa mwasilishaji mzuri

ii. awe na utaratibu na mpangilio wa kiwango cha juu

iii. ni muhimu awe mstahimilivu

iv. ni sharti awe na ujuzi wa kufundisha

v. anafaa kuwa na uhusiano mzuri na wanagenzi

vi. anastahili kuwa na maarifa kuhusu somo husika.

Pamoja na hayo mwanagenzi anayejifunza lugha anapaswa kuwa na sifa zifuatazo:

i. ni sharti awe tayari kujifunza lugha ya Kiswahili bila kulazimishwa

ii. anapaswa kufanya mazoezi mara kwa mara ya kuitumia lugha hiyo

iii. ni sharti awe na maarifa ya kumwezesha kupambanua dhana mbalimbali ili kugundua mambo ambayo jamii fulani inayafanya

iv. anafaa awe na uhuru wa kuzungumza lugha hiyo

v. ni muhimu awe na ratiba ya kujifunza

vi. anastahili kulinganua na kulinganisha lugha anayojifunza

vii. mwanagenzi anafaa kuwa na ukarimu ili aweze kuwa na uhusiano na jamii husika

viii. ni sharti awe mtendaji

ix. mwanagenzi hana budi kuzingatia ubora ili aweze kujifunza zaidi.

 

You can share this post!

Sarri aomba ruhusa atoke Chelsea upesi

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Motisha katika kusoma na...

adminleo