• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
Mbunge atahadharisha kuhusu mkutano wa Uhuru na Raila

Mbunge atahadharisha kuhusu mkutano wa Uhuru na Raila

Na VICTOR RABALLA

MBUNGE wa Nyando Jared Okello amemtaka Rais Uhuru Kenyatta na Kiongozi wa NASA Raila Odinga, wafanye mazungumzo ya wazi ili kukomesha mzozo wa kisiasa uliopo.

Alitahadharisha dhidi ya kutofichua maelezo ya mazungumzo baina yao akisema kuwa huenda yakaibua shauku miongoni mwa Wakenya.

Akizungumzia mkutano huo wa jana baina ya viongozi hao wawili, mbunge huyo wa Nyando alielezea haja ya kuendesha mazungumzo yenye mpangilio ambayo yataunganisha Wakenya ambao wamegawanyika sana baada ya marudio ya uchaguzi wa urais uliosusiwa hasa na watu kutoka ngome za upinzani.

“Tunahimiza pande za Bw Kenyatta na Bw Odinga ziwe wazi kwa Wakenya na kufichua mazungumzo yao yanahusu nini,” alisema.

Aliongeza, “Mazungumzo hayo lazima yajumuishe haki katika uchaguzi na kuvunjwa kwa tume ya sasa ya uchaguzi (IEBC) inayoongozwa na Bw Wafula Chebukati.

Bw Okello alisema hayo akiwa Kisumu, huku akitaja kuwa mzozo wa sasa wa kiuchumi na kifedha umetokana na tume ya uchaguzi kukosa kuendesha uchaguzi huru, wenye usawa na wa kuaminika.

Gavana wa Kisumu Anyang’ Nyong’o alikataa kuzungumzia suala hilo akisema bado hajakutana na kiongozi wa chama cha ODM.

“Habari nilizo nazo bado ni za faragha lakini naweza kukuhakikishia kuwa mkutano huo ulinuia mema kwa Wakenya wote,” alisema.

 

You can share this post!

Wiper yasema Raila alisaliti NASA kukutana na Rais Kenyatta

Ni usaliti mkubwa Raila kukutana na Uhuru – Miguna...

adminleo