Na MARY WANGARI
NI sharti kama mwalimu uwe na maarifa kuhusu tamaduni na itikadi za wanajamii mbalimbali kama vile Wazungu, Wachina, Waarabu na kadhalika.
Ili kufanikiwa katika ufundishaji wa darasa mseto, ni muhimu kuzingatia mambo yafuatayo:
Ni sharti uwe na usisitizaji wa lugha lengwa. Kwa mfano, kama ni lugha ya Kiswahili basi pendelea kutumia Kiswahili ili usiwakwaze sana. Hata hivyo lazima wawe na lugha ambayo wewe unaijua
Tumia vitendo halisi, mathalani ishara na kadhalika.
Toa mwaliko kwa wageni mbalimbali ili waje waeleze kuhusu lugha na mazingira.
Wakati mwingine utahitajika kupuuza malengo ya wanafunzi.
Zingatia kwamba ufundishaji wa masuala ya utamaduni ni sharti ufungamane na muktadha husika.
Sifa za mpataji lugha
Mpataji lugha ni lazima awe na sifa kuu mbili ambazo ni:
1. Umilisi wa kiisimu
Huu ni uwezo alio nao mtu anayejifunza lugha ambao unamwezesha kutofautisha viambo, miundo tofauti ya lugha na msamiati wa lugha
Aidha, ni kuwa na uwezo wa kuitamka lugha ile.
2. Umilisi wa kiisimujamii
Hii ni aina ya umilisi wa lugha ambapo mtumiaji wa lugha hupata lugha inayomwezesha kujifunza lugha na kuzingatia muktadha.
Nadharia, mbinu na mikabala husika katika kujifunza lugha ya pili
Dhana ya nadharia inarejelea mkondo wa mawazo unaotumika kuelezea jambo fulani.
Kwa mujibu wa Mtesigwa (2009), nadharia ni kiunzi cha mitazamo, mawazo au vitendo vinavyohusisha uchunguzi, mpangilio na uchanganuzi wa matukio katika kukabili suala fulani kisayansi. Kwa mintarafu hii, ni vyema tutilie maanani mambo haya mawili:
Njia za ufundishaji lugha ya kigeni ni tele sawia na walimu walivyo wengi.
Zingatia hali ya darasa. Tumia njia au mbinu zaidi ya moja darasani. Usitumie njia moja tu.
Kwa upande wao Rogers & Richards (2001), wanasema kuwa tunapojiandaa kwenda kufundisha tunahitaji kujiuliza maswali yafuatayo:-
Marejeo
Msanjila, Y. P. (1990). “Problems of Teaching Through the Medium of Kiswahili in Teacher Training Colleges in Tanzania”. Journal of Multilingual and Multicultural Development II/4:307 – 318
Mtembezi, I. J. (1997). Njia Mbili Zilimshinda Fisi: Tanzania na Suala la Lugha yaKufundishia. Dar es Salaam: BAKITA.