• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 7:55 PM
Nigeria kuingia uwanjani dhidi ya limbukeni Burundi mechi ya ufunguzi Kundi B

Nigeria kuingia uwanjani dhidi ya limbukeni Burundi mechi ya ufunguzi Kundi B

Na MASHIRIKA

CAIRO, Misri

NIGERIA watajibwaga uwanjani saa mbili usiku Jumamosi katika uwanja wa Alexandria dhidi ya limbukeni Burundi ambao hii itakuwa mara yao ya kwanbza kushiriki katika michuano ya AFCON, lakini itakuwa mara ya 18 kwa mabingwa hao wa zamani.

Mechi hiyo itachezewa Alexandria Stadium ambao una uwezo wa kuchukua mashabiki 20,000.

Nigeria ambao wamepangiwa Kundi B wanajivunia ushindi mara tatu, nishani za fedha nne na moja ya shaba.

Baada ya kutwaa ubingwa huo kwa mara ya tatu nchini Afrika Kusini mnamo 2013, Super Eagles ilishindwa kufuzu kwa michuano ya 2015 nchini Equatorial Guinea pamoja na ile ya 2017 nchini Gabon, lakini raundi hii walifuzu mapema ikisalia mechi moja.

Kocha wao, Gernot Rohr ameeleza kikosi chake kuwa cha wanasoka chipukizi ambao wana hamu kuu ya kutwaa ubingwa.

Baada ya miaka sita, ni wachezaji watatu pekee ambao wangali kwenye kikosi hicho ambao ni nahodha Mikel John Obi, naibu wake Ahmed Musa na mlinzi Kenneth Omeruo ambao walikuwa katika kikosi cha ushindi wa 2013.

Kikosi cha Nigeria kina makipa: Francis Uzoho (Anorthosis Famagusta, Cyprus); Ikechukwu Ezenwa (Katsina United); Daniel Akpeyi (Kaizer Chiefs, Afrika Kusini)

Walinzi ni: Olaoluwa Aina (Torino FC, Italia); Abdullahi Shehu (Bursaspor FC, Uturuki); Chidozie Awaziem (Caykur Rizespor, Uturuki); William Ekong (Udinese FC, Italia); Leon Balogun (Brighton & Hove Albion, Uingereza); Kenneth Omeruo (CD Leganes, Uhispania); Jamilu Collins (SC Padeborn 07, Ujerumani).

Viungo ni: Mikel John Obi (Middlesbrough FC, Uingereza); Wilfred Ndidi (Leicester City, Uingereza); Oghenekaro Etebo (Stoke City FC, Uingereza); John Ogu (Hapoel Be’er Sheva, Israel)

Washambuliaji ni: Ahmed Musa (Al Nassar FC, Saudi Arabia); Victor Osimhen (Royal Charleroi SC, Ubelgiji); Moses Simon (Levante FC, Uhispania); Henry Onyekuru (Galatasaray SK, Uturuki); Odion Ighalo (Shanghai Shenhua, China); Alexander Iwobi (Arsenal FC, Uingereza); Samuel Kalu (Girondins Bordeaux, Ufaransa); Paul Onuachu (FC Midtjyland, Denmark); Samuel Chukwueze (Villarreal FC, Uhispania).

 

Imetafsiriwa na John Ashihundu

You can share this post!

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Mambo yanayoathiri mchakato wa...

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Tofauti za upataji wa lugha ya...

adminleo