• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 10:15 AM
FUNGUKA: ‘Napashwa joto na jini’

FUNGUKA: ‘Napashwa joto na jini’

Na PAULINE ONGAJI

KWA muda sasa, kumeibuka kejeli nyingi mtandaoni kuonyesha jinsi mtoto mvulana – boy child – amekuwa akihangaika mikononi mwa mabinti hasa katika masuala ya mapenzi.

Ni suala ambalo limewafanya wanaume wengi kuonyesha wazi chuki dhidi ya mabinti huku baadhi yao wakisisitiza hawana haja ya kuwachumbia.

Ousman, 33, alikata kauli hiyo akiwa na miaka 19 pekee, wakati huo akiwa katika shule ya upili.

Hata hivyo uamuzi wa jamaa huyu mkazi wa eneo la Pwani ya Kenya haukutokana na machungu kutokana na binti, bali aliamua kufanya hivyo baada ya kuonja utamu wa jini wa kike, kama anavyosimulia.

“Maishani mwangu sijawahi kuwa katika uhusiano wala kufurahia mahaba na binti mwanadamu. Huyu jini wangu tulikutana naye miaka 14 iliyopita baada ya kutambulishwa na mwenzangu ambaye kwao walikuwa wamefuga viumbe hawa.

Yeye ni mrembo ajabu ambapo tangu nimjue hajawahi kuzeeka. Umbo lake ni lile lile; tumbo bapa, kifua thabiti na kiuno cha mviringo. Uke wake ni thabiti kabisa, licha ya kuwa tumekuwa tukirushana roho kwa zaidi ya mwongo mmoja.

Nilimuonja kwa mara ya kwanza nikiwa na umri wa miaka 19 nikiwa ningali kushiriki tendo lenyewe la kuonana kimwili na yeyote na hapo nikaamua kwamba ni yeye tu sitaki mwingine.

Jini wangu huja usiku wa manane akiwa uchi wa mnyama ambapo akiingia kwenye fleti ninamoishi, hakuna jirani anayemuona wala kumsikia.

Akifika, sisi hutekenyana kwa saa nzima na kuzungumza kwa muda wa saa kadha kabla yeye kurejea majini.

Uhondo anajua kunipa na ninachofurahia ni kwamba yeye ni mungwana kiasi kwamba tukishamaliza, husafisha kila mahali na kuhakikisha kwamba anaacha kila kitu alivyokipata.

Mbali na hayo, licha ya kwamba hakuna kinga tunayotumia, sina wasiwasi wa kuambukizwa maradhi ya zinaa, wala hatari ya mimba isiyotarajiwa.

Sisi hushiriki mahaba mara tatu kwa wiki; Jumanne, Ijumaa na Jumapili, na nyakati zote huwa saa tisa za usiku.

Aidha, sina ajira wala mbinu yoyote ya kujitafutia riziki, lakini naishi maisha kama mfalme, nina nyumba na magari kadha ya kifahari anayoninunulia.

Sihitaji kufanya kazi kwani hunipa pesa pia. Nabadilisha simu kila mara bila wasiwasi. Kila ninapochoshwa na niliyonayo, mimi humrejeshea kisha ananiletea mpya.

Nina fanicha na vyombo vya kisasa ndani ya nyumba yangu na mali nyingi kutoka kwake na asema hufanya hivi kunizuia kuingia kwenye mtego wa mwanamke yeyote binadamu.

Pia, amenionya kwamba nikiwahi kuonja vya binadamu nitayaona matokeo ambayo hajawahi nifichulia. Lakini mwenyewe sifikirii kutafuna vya binadamu kwa sababu uhondo anaonipa umenilewesha”.

You can share this post!

OCS motoni kumruhusu Itumbi kustarehe seli

MWANAMUME KAMILI: Acha wakuite zumbukuku ila wasijue...

adminleo