• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Starlets wasalia 108 duniani viwango vya FIFA

Starlets wasalia 108 duniani viwango vya FIFA

Na GEOFFREY ANENE

HARAMBEE Starlets ya Kenya imekwamilia nafasi ya 108 kwenye viwango bora vipya vya soka ya wanawake duniani vilivyotangazwa na Shirikisho la Soka duniani (FIFA), Ijumaa.

Wapinzani wa Kenya katika mchuano wa kirafiki utakaopigwa Machi 25, Shepolopolo ya Zambia, wameteremka nafasi mbili hadi nambari 98 duniani.

Kenya, ambayo inanolewa na makocha David Ouma na Richard Kanyi, iliondoka nchini Alhamisi mapema asubuhi kuelekea Zambia kwa mchuano huo utakaochezewa mjini Kitwe.

Starlets itatumia mechi hii kujipiga msasa kabla ya kupepetana na Uganda kutafuta tiketi ya kushiriki Kombe la Afrika mwaka 2018 litakaloandaliwa nchini Ghana kutoka Novemba 17 hadi Desemba 1.

Kenya itaalika Uganda hapo Aprili 4 kabla ya kuelekea ugenini kwa mechi ya marudiano mnamo Aprili 8.

Uganda imeshuka nafasi saba katika viwango bora vya FIFA. Iko katika orodha ya mataifa ambayo hayajajishughulisha kusakata mechi za kimataifa kwa zaidi ya miezi 18.

Mechi ya mwisho ya Kenya ya kimataifa ilikuwa dhidi ya Zambia mnamo Septemba 23, 2017. Starlets, ambayo ilikuwa imealikwa kushiriki mashindano ya Afrika ya Kusini (Cosafa) nchini Zimbabwe, ililemewa 4-2 na Zambia kwa njia ya penalti katika mechi ya kutafuta mshindi wa medali ya shaba baada ya muda wa kawaida kumalizika 1-1.

Kabla ya kupigwa breki na Zambia, Kenya ilikuwa imetesa katika mashindano hayo kwa kuzaba Msumbiji 5-2, Mauritius 11-0 na Swaziland 1-0 katika mechi za Kundi B. Ilipepetwa 4-0 na Zimbabwe katika nusu-fainali.

Vikosi:

Kenya

Makipa – Pauline Atieno, Maureen Shimuli;

Mabeki – Dorcas Shikobe, Wendy Achieng, Carolyne Anyango, Lilian Adera, Vivian Nasaka, Esther Nadika, Pauline Musungu, Wincate Kaari;

Viungo – Cheris Avilia, Dorris Anyango, Sheryl Angachi, Caroline Kiget, Corazone Aquino;

Washambuliaji – Mwanahalima Adam, Mercy Achieng, Phoebe Owiti, Neddy Atieno, Cynthia Shilwatso.

Zambia

Makipa – Catherine Musonda, Annie Namoonje, Bupe Mwanza, Maleta Muwindwa, Yolanta Haankanga;

Mabeki – Jacqueline Nkole, Margaret Belemu, Mercy Nthala, Lweendo Chisamu, Jane Chalwe, Esther Siyafukwe, Mweemba Lushomo;

Viungo – Mary Mwakapila, Maylan Mulenga, Hellen Chanda, Rachael Lungu, Prisca Chilufya, Rabecca Nyirenda, Rexina Lutaka, Mary Mambwe, Rhoda Chileshe, Aliness Kasoma, Womba Chimuachi;

Washambuliaji – Misozi Zulu, Racheal Kundananji, Theresa Chewe, Agness Musesa, Avel Chitundu, Lydia Mubanga, Muyoi Luwi.

You can share this post!

Itawabidi Stars kujikakamua zaidi kuzima Comoros na CAR,...

Matano aitaka Ingwe imfidie Sh4.9 milioni kwa kumsimamisha...

adminleo