• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:05 AM
Odera ataja kikosi cha Simbas kukabiliana na Zimbabwe raga ya Victoria Cup

Odera ataja kikosi cha Simbas kukabiliana na Zimbabwe raga ya Victoria Cup

Na GEOFFREY ANENE

KENYA imetangaza kikosi chake cha Simbas kitakacholimana na Zimbabwe katika mechi ya mwisho ya raga ya wachezaji 15 kila upande ya Victoria Cup uwanjani Nakuru Athletic mjini Nakuru hapo Septemba 21.

Kocha Paul Odera amejumuisha Joshua Chisanga, ambaye amekosa mechi mbili zilizopita dhidi ya Uganda, mbili dhidi ya Zambia na Zimbabwe (moja) kwenye Victoria Cup.

Chisanga alichezea Kenya mara ya mwisho katika mchujo wa mwisho wa kuingia Kombe la Dunia uliokutanisha Kenya dhidi ya Canada, Ujerumani na Hong Kong mwezi Novemba mwaka 2018 nchini Ufaransa.

Kenya ilichapwa 30-29 na Zimbabwe ilipozuru mjini Bulawayo kwa mechi ya mkondo wa kwanza mwezi Agosti na itatumai itafanikiwa kulipiza kisasi dhidi ya Zimbabwe, ambayo imeshinda mechi zake tano zilizopita.

Simbas ilianza kampeni kwa kulimwa na Uganda 16-13 mjini Kisumu kabla ya kulipiza kisasi 16-5 jijini Kampala na kisha kupepeta Zambia 43-23 mjini Kitwe na kupoteza 30-29 dhidi ya Zimbabwe kabla ya kunyamazisha Zambia 31-16 jijini Nairobi mnamo Agosti 24.

Kikosi cha Kenya Simbas: Wachezaji 15 wa kwanza – Ian Njenga, Toby Francombe, Melvin Thairu; Emmanuel Mavala, Malcolm Onsando; Joshua Chisanga, Monate Akuei, Elkeans Musonye; Samson Onsomu (nahodha), Charles Kuka; John Okoth, Vincent Onyala; Timothy Okwemba, Geoffrey Okwach na Anthony Odhiambo.

Wachezaji wa akiba – Frank Mutuku, Elisha Koronya, Ian Masheti, Brian Juma, Samuel Were, Barry Robinson, Tony Omondi na Michael Kimwele.

You can share this post!

Nema yafunga kiwanda cha karatasi za nailoni Juja

Sonko anavyokwepa kukamatwa na DCI

adminleo